Ujumbe wa Papa kwa Mkutano wa Dunia wa Viongozi wa Kidini, unasema vita haina maana
kwa kuwa haiwezi kurekebisha tatizo la ukosefu wa haki. Haki hupatikana katika kuheshimiana,
mazungumzo na ushirikiano, hizo ndizo silaha zinazofaa kudumisha haki na maridhiano.
Ni maneno ya mazito yaliyomo katika ujumbe Papa, kwa mkutano wa kila mwaka
unao andaliwa na Jumuiya ya Sant'Egidio. Mkutano huo kwa mwaka huu, unafanyika chini
ya Madambiu"Amani ni siku zijazo. Ujumbe wa Papa Francisko ulisomwa
kwa washiriki wa Mkutan, siku ya Jumapili mchana , wakati wa sherehe za ufunguzi
wa mkutano huo, unao fanyika mjini Antwerp, Ubelgiji. Mkutano unakamilika Jumanne
hii.
Francesca Sabatinelli, wa Redio Vatican, ametaarifa tokea mkutano, na
kwamba, Papa umetaja mizozo yenye kusababisha umwangaji wa damu, inayoshuhudiwa siku
hizi, unawarejesha washiriki kutafakari kwa kina somo lililotolewa kwa dunia, kutoka
Vita vya dunia ambavyo vimetimza miaka miaka mia, tangu kuzushwa.
Maadhimisho
haya - anasema Papa Francisko, yanatoa somo kwamba, vita kamwe si njia inayofaa
kuondoa madhulumu na kutotendewa haki. Ni tu katika njia ya mashaurianao na maridhiano,
huweza kumaliza ugomvi wa kisiasa na kijamii kwa amani. Kila vita, aliongeza kwa
kumnukuu Benedict XV katika waraka wake wa mwaka 1917, huwa ni umwangaji wa damu
usiokuwa na maana. Vita huwaweka watu katika mduara wa hali ngumu na vurugu ambazo
udhibiti wake unakuwa mgumu , na hivyo kuvuruga mema na maendeleo yote yaliyokwisha
jengwa na wahenga. Vita ni njia ya udhalimu yenye kujenga migogoro zaidi.
Papa
alieleza bila ya kutaja eneo lolote lenye kuwa na migogoro na vita kwa wakati hii,
lakini alisema vita vinavyoendelea leo hii vinachoma mioyo ya watu, na vina angamiza
maisha ya vijana na wazee. Vita ni sumu ya mshikamano wa makundi ya kikabila na kidini,
vyenye kulazimisha jamii nzima kuishi uhamishoni, ambako wanapambana na mateso bila
ya huruma, wengi wakipoteza maisha. Hapa ndipo, tunaona maana ya hatua hii ya kuunganisha
viongozi wa dini mbalimbali, kujumuika pamoja katika Roho wa Assisi, kwa nia ya kutoa
mchango kwa amani duniani, kupitia njia ya maombi ya pamoja na mazungumzo.
Papa
amesisitiza vita -havina maana yoyote, na vinaweza kuepushwa. Daima inawezekana kupata
mbadala kupitia njia ya mazungumzo na tafiti za dhati na kweli katika kupata jawabu
linalofaa wote.
Kwa hiyo Francesko, amewaomba viongozi wa dini walio kusanyika
Ubelgiji, kufanya kazi kwa ushirikiano wa dhati kwa ajili ya ufanisi katika matendo
ya kuponya majeraha, kutatua migogoro inayokera wanaume na wanawake, kwa njia ya
amani. Jumuiya zetu, ujumbe unahitimisha, ni “shule” ya heshima na mahali pa mazungumzo
na wote, kikabila au kidini na makundi mengine. Ni eneo ambapo tunajifunza kushinda
mvutano, na kukuza mahusiano ya usawa na amani kati ya watu na makundi ya kijamii
na kujenga dunia iliyo bora ya baadaye kwa vizazi vijavyo. Na huo ndiyo ujumbe msingi
wa mkutano huu ulioandaliwa na Jumuiya ya Mtakatifu Egidio kila mwaka.