2014-09-06 09:49:13

Masista wa SOM, wanaendelea na Mkutano wao Mkuu wa 44


Mjini Loreto tangu tarehe 24 Agost hadi 14 Septemba 2014, Masista wa Huruma ya Wahudumu Hospitalini(SOM), wanaendesha Mkutano wao Mkuu wa 44 juu ya mada: Huruma na shufaka – Moyo wa Karama yetu.

Mkutano huu ulioanza na mafungo ya kiroho kwa muda wa wiki moja, unahudhuriwa na wajumbe Masista 31 kutoka India, Ufilipino, Marekani, Madagascar, Nigeria, Italia na Poland, na unafanyika katika Taasisi ya Mtakatifu Yosefu ya Loreto ya hapa Italia, kwa ajili ya kuandaa mipango ya utekelezaji kwa shirika katika kipindi kingine cha miaka sita ijayo, ikiwa pamoja na uchaguzi wa Mama Mkuu Mpya wa shirika na wajumbe wawakilishi wa Shirika hilo. Shughuli za shirika hili hasa zinazolenga katika uwanja wa afya zilianza, miaka 193 iliyopita. Wajumbe wa mkutano unaoendelea wanatazamia kukutana na Papa Francisco hapo tarehe 17 Septemba, mjini Vatican.

Shirika la SOM, ambako kwa wakati huu lina wanashirika Masista 400, linaongozwa kwa wakati huu na Mama Mkuu Paola Iacovone, lilianzishwa hapa Roma na Binti Mfalme Teresa Orsini Pamphili Land mwaka 1821, na kuwa Shirika la kwanza la watawa wa kike kuhudumu hospitalini katika jiji la Roma.Na pia walikuwa ni Masista wa kwanza kuhudumia Hospitali Kuu ya Mtakatifu Salvatore ambayo sasa ni inajulikana kama Hospitali ya Mtakatifu Yohane wa Mateso. Karama ya masisita hawa ni kutoa msaada kwa jamii ya leo inayokabiliwa na mateso ya mwili na kisaikolojia hasa kwa wagonjwa wanaolazwa hospitalini.

Pia kati ya shughuli katika utume wao ni kutoa msaada kwa chama cha watu wa kujitolewa katika masuala ya afya”La Cometa Onlus” kilichoanzishwa mwaka 2003, kwa pamoja na kikundi cha Walei wanaojishughulisha na kazi za kukusanya fedha nakukuza mipango ya uratibu kati ya masisita waliotawanyika pande mbalimbali za dunia, ikiwemo mipango ya kupanga watoto tokeo maeneo ya mbali.

Na hivyo karibuni kumezaliwa tawi jipya la chama kinachojulikana kama Teresa Orsini , lililoanzishwa huko Gravina Puglia , aliko zaliwa mwanzishi wa Shirika la SOM, ambacho kinajishughulisha pia na malezi ya kiroho kwa Wamama vijana.

Na pia inaelezwa kwamba, mchakato unaotafuta kumtaja kuwa Mwenye Heri mwanzilishi wa SOM, katika historia ya shirika hili tayari umeanza na pia wanaye Mwenye Heri Sisita Raffaella Cimatti, aliyetangazwa kuwa Mwenye Heri na Na Mtakatifu Papa Yohane Paulo II.








All the contents on this site are copyrighted ©.