2014-09-05 16:13:07

Papa akutana na Shimon Peres na Mwana Mfalme wa Jordan


(Vatican Radio) Papa Francisko, AlhamIsi asubuhi, alikutana katika mazungumzo ya faragha na watu mashuhuri wawili, Rais wa zamani wa Israeli, Shimon Peres, na mwingine Mwana Mfalme El Hassan bin Talal wa Jordan.
Padre Federico Lombardi, SJ, Mkurugenzi wa Ofisi ya Habari Vatican, aliwapa taarifa fupi wanahabari kwamba, Rais wa zamani Peres aliomba kukutana na Papa hasa kwa ajili ya kumfahamisha Papa shughuli zake na miradi yake kwa ajili ya amani, ikiwemo mpango wa pamoja wa kuwashirikisha vijana katika michezo katika miji ya Israel na Palestina, ambamo zaidi ya watoto themanini watashiriki, katika nyakati mbalimbali kama itavyokuwa imeandaliwa mwaka kwa mwaka, na taasisi ya muungano wa dini, iliyobuniwa na Umoja wa Mataifa.
Akizungumza na Radio Vatican baada ya mkutano huo,Padre Lombardi aliutaja mkutano wa Papa na Rais wa zamani wa Israel kwamba ulidumu takribani dakika 45, na Papa alimsikiliza kwa makini na kueleza mawazo yake pia juu ya mpango wa Rais Peres, na kumhakikishia kwamba Idara husika za Curia ya Roma zitatoa ushirikiano wa hali ya juu, hasa zinazohusika na amani na maridhiano kati ya tamaduni na dini mbalimbali, na hasa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Mazungumzo kati ya dini, na Baraza la Kipapa kwa ajili ya Haki na Amani, na Makardinali Tauran na Peter Turkson.

Kuhusu pendekezo la Rais wa zamani Peres, kuunda Taasisi ya kuunganisha dini "United Religions", Padre Lombardi amesema ni mada iliyojadiliwa katika mkutano wa viongozi hawa kwa makini, na pia ilikuwa kama nafasi ya kupitia upya mkutano wa kihistoria katika Vatican, wakati Rais Peres na Rais wa Palestina Mahmoud Abbas, waliposhiriki katika mkutano wa sala ya amani hapa Vatican, juhudi ambazo haziwezi kutajwa kama zilishindwa kwa kuwa zinaendelea kufanyiwa kazi na hivyo imekuwa kama ni kufungua mlango wazi, kwaajili ya kuanzisha juhudi mbalimbali katika lengo hilo la ujenzi wa amani na maridhiano, kwa njia ambayo juhudi na maadili vinaweza kuwa moyo wa kusonga mbele na hatua hizo, jambo lililosisitizwa na Papa Francisko hata baada ya kukutana na Rais Peres.

Na juu ya Papa kukutana na Mwana Mfalme Hassan wa Jordan, Padre Lombardi alieleza kwamba, ulikuwa ni muhimu pia na katika mtazamo huohuo wa kuwasilisha kazi kuwasilisha kazi zaTaasisi yenye utendaji wenye mwingiliano wa dini, tafiti za tamaduni na majadiliano iliyoanzishwa na Mwana Mfalme ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza, pia kama ilivyo kwa Taaisisi ya Kifalme ya tafiti kati ya dini mbalimbali , ambayo pia aliianzisha Mwana Mfalme Hassan. Shuguli za taasisi hizo zote zimeelekezwa katika kufanikisha majadiliano kati ya dini na dhamira ya amani, katika mazingira ya sasa ya vurugu. Na hivyo kunakuwa na umuhimu wa kipekee kufanikisha majadiliano baina ya dini kwa heshima ya binadamu na amani, na kusaidia masikini katika wakati wa utandawazi, elimu kwa vijana, ushirikiano katika udugu, na msisitizo juu ya heshima na hadhi ya binadamu wote.

Aidha Padre Lombardi, alitoa taarifa fupi juu ya safu ya mada nyingine, ikiwa ni pamoja na mkutano wa Baraza la Uchumi la Vatican - uliofanyika Alhamisi, ili kuchunguza masuala ya kisheria, kiufundi yanayohusiana na mageuzi ya taasisi Vatican kiutawala na ya kifedha - na uwezekano wa mkutano kati ya gavana wa Usharika kwa Mafundisho ya Imani, Kardinali Gerhard Mueller, na Mkuu wa Udugu wa Matakatifu Pius X, Askofu Bernard Fellay, ambao tarehe yake bado kujulikana.








All the contents on this site are copyrighted ©.