2014-09-05 09:27:16

Mtandao wa kimataifa kwa ajili ya elimu wazinduliwa Vatican


(Vatican Radio) Baba Mtakatifu Francisko, alikutana na Wakurugenzi wa Taasisi ya Kimataifa kwa ajili ya mtandao wa elimu inayojulikana kwa jina "Scholars Accurents", yenye Makao yake makuu huko Argentina, ambalo hulenga kuunganisha shule na mitandao ya elimu kutoka tamaduni na imani mbalimbali. Taasisi hii ilikuwa ni kati ya waliofadhili tukio la Mechi ya mpira kwa ajili ya amani, siku ya Jumatatu katika uwanja wa michezo wa Olympic hapa Roma.

Baba Mtakatifu Alhamis akizunguza kwa njia ya Video, alirudia kuwashukuru Wakurugenzi wa Taasisi hii ya Scholars Accurentes kwa mafanikio yaliyokwisha patikana na aliwahimiza kuendelea na juhudi zao katika ujenzi wa mwingiliano kati ya tamaduni mbalimbali za kidini na elimu, na hivyo kuwa kama daraja la maelewano na udugu. Papa alitaja thamani ya ujenzi wa madaraja na kusikiliza, katika dunia yenye kuwa na vita na ghasia kama zinazosikika, na kutoa wito wa kutowaacha watoto peke yao.

Baba Mtakatifu pia alifanya mkutano wa video kupitia mtandao na wanafunzi katika nchi mbalimbali juu za mabara 5: Salvador, Afrika Kusini, Ulaya Uturuki (Istanbul), Israel, Australia, Cameroon. Papa pia alijibu maswali ya wanafunzi.
Baba Mtakatifu Francisco, amezidua jukwaa la kimataifa la Digital kwa ajili ya kuziunganisha shule mbalimbali duniani ambamo teknolojia, sanaa na michezo vinaweza kutumiwa katika kuhimiza utamaduni wa kukutana na mwingiliano wa tamaduni hasa vijana.

Baba Mtakatifu Francisko anaamini kuwa ni muhimu kuhamasisha utamaduni wa kukutana. Na hivyo jukwaaa hili limeandaliwa katika mtazamo wa uadilifu wa dini katika maisha ya kila siku. Na kwamba , juhudi hizi za "Scholas Occurrentes, zinatoa mwaliko kwa wenye taaluma mbalimbali, kama madaktari, polisi, walimu , na hata vijana wasiokuwa na ajira, kukutana kwa njia hii ya digital, kwa ajili ya kukuza mawasiliano katika kupeana ujumbe wa amani. Papa anaamini njia hii itaweza kuwaunganisha watoto na vijana wengi kwa mfano katika uwnaja wa michezo sanaa ambazo ni njia kuu katika majiundo ya kuzingatia tunu za heshima ya utu wa mtu.

Wakurugenzi wa juhudi hizi za Scholas duniani, José Maria del Corra na Enrique Palmeyro, wakizungumza na wanahabari wanasema, juhudi hizi walisema, zinavutia kwa sababu, zimezaliwa na mpango wa awali wa Papa akiwa bado Askofu Mkuu wa Buenos Aires, alifanya majaribio ya kujenga mtandao wa shule katika misingi ya teknolojia, michezo na sanaa, kuwa na mafanikio. Na Papa aliwaomba wanaoendesha mpango huu huko Buenos Aires, kuendeleza mradi huu duniani kote. Tarehe 19 Machi, kulifanyika mkutano na Papa mjini Vatican na hapa baada ya mchezo wa amani kati ya madhehebu, kama ilivyokuwa imeandaliwa na “ Scholas Foundation na Argentina PUPI Onlus”. Mkutano huo umefuatiwa na mkutano mwingine wa siku ya Jumatano wiki hii katika ukumbi wa sinodi wa hapa Vatican. Na Alhamisi, Papa Francis wa Wajumbe wa taasisi hii, katika ukumbi wa wa Sinodi, ambamo Papa alizungumza na kuweza kufuatiliwa na shule zilizo katika mtandao huu katika bara tano.

Papa analenga hasa kutumia matukio ya mechi za michezo, sanaa, na hasa teknolojia, kusaidia utamaduni wa mkutano na juu ya matukio hayo badala ya kwenda vitani , na kumsaidia kijana kukua kama ndugu, lakini bila ya kupoteza utambulisho wa utamaduni au dini yake. Ujumbe wa Papa unasema, "Kuna vita ya kutisha yenye kuharibu ubinadamu: hii basi ni jaribio la kuleta pamoja vijana na hata watu wazima katika kujenga pamoja utamaduni kukutana watu mbalimbali kwa amani".

Mtandao huu ni kwa nchi zote nchi tajiri na maskini, na jukwaa linalokwenda katika nchi zote za dunia. Ni mpango ambayo inatoa uwezo wa kushiriki na kuungana na wote bila ya ubaguzi wa kidini , kitaifa au kimbali. Ni jukwaa la kuwaunganisha wote kwa amani.










All the contents on this site are copyrighted ©.