2014-09-03 16:04:38

Kanisa, Mama wa Wabatizwa wote


Kanisa ni mama mwenye kuonea fahari watoto wake. Hili limeelezwa na Papa mapema Jumatano, wakati akitoa katekesi yake kwa mahujaji na wageni walio fika kumsikiliza katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro Vatican. Katika Katekesi hiyo Papa pia kwa namna ya pekee, aliwakumbuka Wakristo wanaoteseka, hasa huko Iraq nakuwakumbusha kwamba, Kanisa kwa maombezi ya Bikira Maria Mama wa Kanisa, daima huwatetea watoto wake , na kuteseka pamoja nao katika dhiki zao zote.

Baba Mtakatifu Francisco katika Katekesi hii kwa mahujaji na wageni, aliendelea kutafakari juu ya Imani ya Mkristo kama alivyosiistiza kwa mara kadhaa kwamba, haiwezekani kuwa Mkristo wa kweli kwa kujitenga mbali na wengine, au kwa kutumia nguvu binafsi za kibidamu na ukristo hautengenezwi katika maabara , lakini kwa yale yanayotokana na matendo mema na kukua katika imani inayowaunganisha waumini wote katika mwili mmoja ambalo ni Kanisa. Kwa maana hii, Kanisa linakuwa kweli mama, mama yetu Kanisa. Papa alisisitiza akisema , tazama tu hata inavyo pendeza kutamka, Kanisa ni mama yetu, ndiye anayetupatia uhai katika Kristo na hutufanya kuishi kama ndugu katika umoja wa Roho Mtakatifu.

Papa alitoa mada yake chini ya vipengere 3. Kwanza alilizungumzia umama wa Kanisa, kwa mfano wa Bikira Maria, mfano ulio bora kuliko mifano yote inayoweza kutolewa, akiangalisha katika maelezo yaliyotolewa na Wakristo wa mwanzo na pia kwa mwanga wa Mtaguso Mkuu wa Pili a Vatican (cf. Const. Lumen Gentium, 63-64).Umama wa Maria ukionekana kuwa hakika ni wa kipekee, uliokamilishwa na utimilifu wa wakati, wakati Bikira alipojifungua Mwana wa Mungu, kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Papa aliendelea kueleza juu ya mwendeleza wa uhusiano huu wa Mama Bikira Maria na Kuzaliwa kwa Kanisa alilolibeba tumboni mwake, akisema kweli ulikuwa ni mwanzo wa kuzaliwa upya kwa kila Mkristo katika tumbo la Kanisa, Kristo akiwa uzao wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi (Rum 8:29) na ndugu yetu wa kwanza, Yesu aliyezaliwa Maria ni mfano wa kuigwa, na sisi wote tulio zaliwa ndani ya kanisa. Tunahitaji kuelewa juu ya uhusiano unaunganisha Maria na Kanisa kwamba , daima hutupa sura nzuri na saburi zaidi katika kulitumainia kanisa, na katika kutambua sifa za uakatifu wa Mama Maria.

Papa alieleza huku akishangiliwa na waliokuwa wakisikiliza kwamba, Sisi Wakristo, si watoto yatima, tuna mama, hili ni neema kubwa. Alisisitiza mara kwamba kwamba, ndani ya Kanisa Wakristo si yatima, kwa kuwa Kanisa ni mama, Maria ni mama.

Pili, Papa alisema, Kanisa ni letu kwa kuwa tumezaliwa ndani yake kwa ubatizo. Na hivyo kila mbatizwa , anakuwa ni mwana wa kanisa , na huingia ndani ya tumbo la kanisa. Na hili linatufanya sisi kukua katika imani na inatuonyesha sisi, kwa uwezo wa Neno la Mungu, njia ya wokovu kwamba tunaweza kujilinda dhidi ya kutenda maovu.

Na tatu , Papa alizungumzia juu ya upendo wa Kanisa , akisema ndani ya kanisa sote tunapendwa kama wana wa mama mmoja, mama ambaye anajali ustawi wa watoto wake hata akiwa tayari kuyatoa maisha yake kwa ajili yao. Papa amekumbusha kwamba kanisa si Maaskofu, au Mapadre au watawa peke yao. Kanisa ni jumuiya nzima ya waamini wabatizwa, kila kubatizwa, mwanaume na mwanamke, na kila lika, vina na watoto pamoja huunda Kanisa.

Papa alikamilisha kwa kuhoji lakini ni mara ngapi katika maisha yetu kama wabatizwa, hatuwezi kumshuhudia mama huyu mkuu Kanisa. Tunahitaji kusali ili kupata ujasiri wa kufanya hivyo. Yesu, anasema, roho wa mama huyu yumo katika usharika , umoja na uwezo wa kujali mahitaji ya wengine , kusamehe, kufariji katika kusimama imara katika matumaini.

Na hivyo tujiweka chini ya Mama Yetu Maria, Mama wa ndugu yetu mzao wake wa kwanza, mwenye kutufundisha kwamba kuipokea roho yake ya kimama ni katika kukutana na ndugu zetu, katika ukweli wa kupokea, kusamehe na majitoleo kwa ajili ya wengine katika uaminifu wa kina na matumaini.

Baada ya Katekesi hii Papa alisalimia makundi mabalimbali ya kijamii, wakiwemo wagonjwa, wanandoa na vijana. Na mwisho kwao wote aliwapa baraka zake za Kipapa.








All the contents on this site are copyrighted ©.