2014-08-27 09:23:44

Maandalizi ya Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya Familia


Katika kuelekea kilele cha mkutano wa maandalizi ya Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya familia, Ijumaa iliyopita 23.08.2014, gazeti la Oservatore Romano lilitoa tafakari juu ya maandalizi ya sinodi hiyo inayotarajiwa kufanyika, Oktoba 2014.

L'0sservatore Romano limeandika kwamba katika maandalizi ya sinodi maalumu ya maaskofu kwa ajili ya Familiaitakayofanyika kuanzia 5 hadi 19 Oct 2014 kuna haja ya kuangalia vipengere muhimu vinavyotokana na desturi ya kanisa, ili sinodi isichambue tu yaliyotoka katika Mabaraza ya Maaskofu Katoliki lakini uwe ni wakati wa kusikiliza hoja zote zilizotolewa na watu wote wa familia ya Mungu, ambao wanaalikwa kushiriki na kuwasindikiza kwa sala katika kazi itakayofanyika .

Na pia limefafanua maana ya Sinodi, ambalo katika kigiriki, ni neno ambalo lilitumika katika Injili ya Mtakatifu Luka analipoelezea juu ya safari ya Maria na Yosefu walipokuwa njiani kumtafuta Yesu akiwa na miaka kumi na mbili na walimkuta katikati ya walimu na waandishi wa ekalu la Bwana , akitenda kazi ya baba yake.Ni neno linalotufanya hata sisi tuweze kutafakari.

Kuhusu tafakari ya kutafutwa kwa Yesu aliyekuwa amepotelea hekaluni, naye
Papa Benedikto wa kumi na sita katika barua yake ya kitume ya Utoto wa Yesu sura ya 141 anaandika kuwa :
Luka anatumia neno synodi, yaani Jumuiya ya safari, akiwa na maana kwamba ni neno la kitaalamu kuwa na maana msafara. Kwa mantiki hii fikira zetu labda tunaweza kusema ni ubahili wa familia takatifu, na pia inawezekana kutushangaza lakini kumbe inatuonyesha maana nzuri ya kwamba katika familia takatifu , uhuru na utiii vilikuwa ni vitu vinavyopatana, vinavyokwenda pamoja.
Mtoto wa miaka kumi na mbili alikuwa ameachwa huru achague , ni namna gani ya kutembea na marafiki zake anaolingana nao wakati wakiwa njiani. Lakini jioni wazazi wake walikuwa wakimsubiri arudi kwao.

Tukiangalia mada ya habari hii tunapata mambo mawili yanayojisuka yenyewe ikiwa na maana yake kuu..yaani tunapofikiria sinodi inayotajiwa kwa maana ya : kutafuta uwepo wa Yesu, ambaye kamwe hajaacha kanisa lake, bali ameungani nalo bila kutenganishwa , ni kama familia yake kweli .Na pia Kanisa lifanya uhusiano na Yesu katika uhuru na utii ili kuacha Roho Mtakatifu ndiye aweze kuelekeza ukweli wa mambo yote. (Joh 16,13).

Ili kuweza kujua zaidi Yesu na ndani ya kanisa, ki ukweli inabidi kujipanga upya na kujiweka katika hali ya usikivu wa neno lake, ambao kadili siku zinavyokwenda na kupitia desturi za kanisa ya kikristo. Tangu enzi za zamani wakati kanisa lilijikuta linapaswa kuchukua uamuzi juu ya matatizo mapya .

Yaliyokuwa yanajitokeza na amabayo hata Yesu alikuwa hakugusia, Kanisa lilijikuta lina sababu ya kutafuta namna ya kufanya na hasa kuweka mafundisho na maelekezo yenye kuwa na msimamo mmoja wa kutekeleza , ili kutatua matatizo hayo mapya., Kwa namna hiyo ikafanyika kanuni na mwongozo ambao ukaweza kutunza imani kwa Bwana wake katika madiliko ya nyakati na tamaduni.
Kwanza ilifanyika sinodi na baadaye mtaguso , hivi ni vIpengere viwili vilivyo fanyiwa kazi kwa umakini na kuweza kupata majibu ya yanayo endana sawia na Maandishi Matakatifu.

Katika harakati za maandalizi ya sinodi kwa ajili ya kutangaza kwa shauku kubwa na uzuri wa Injili ya familia , ya kujibu matumaini yake na kutibu walio umia roho
ni muhimu kukumbuka kwa matumaini ni kitu gani kiliandikwa katika muhutasari wa maadalizi ya sinodi kiitwacho hati ya kufanyia kazi "instrumentum laboris" ya kwamba: “Katika haraka hii ya kanisa kuu la Petro anayejiweka kwa unyeyekevu ya kusikiliza Roho Mtakatifu, akitafakari juu ya changamoto za kitume za leo”

Kwa hiyo hatuna budi kuungana na Jumuiya katika safari , kwa sala , na kuwa na subira ambayo ndiyo inayo lisha amani hili kuamsha upendo , ambao Yesu Kristo anaipelekea kanisa , na imani hiyo ianaendelela kutunzwa kwa uhuru na utii , aliyojifunza kuitii familia takatifu ya Nazareth, ambayo ni kama nyumba ya baba ya kuzaliwa , kwa hiyo hata sisi sote tunayo nafasi huko pamoja na kuwa na maisha magumu.













All the contents on this site are copyrighted ©.