Kambumbu kuchezwa kwa ajili ya kueneza Ujumbe wa amani duniani
Septemba Mosi katika viwanja vya Olympic vya mjini Roma, kutafanyika mashindano ya
mpira wa miguu kati ya timu mbili za kidini kwa heshima ya Papa Francisco, kwa ajili
ya kutoa ujumbe wa nguvu wa amani duniani. Ni mpango uliowasilishwa siku ya Jumanne
kwa wanahabari katika ukumbi wa Makao Makuu ya Redio Vatican. Kati ya walio shiriki
katika mkutano huo ni Msgr. Guillermo Karcher, afisa katika Sekretarieti ya Vatican
kwa ajili ya khafla za Kipapa , mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu Javier Zanetti,
wakiwepo pia wachezaji kutoka timu ya Lazio, Cristian Ledesma,na Juan Iturbe wa timu
ya Roma.
Mchezo huu utakao fanyika katika uwanja wa Olympic Roma, Mosi Septemba
20:45, si mechi za kipinzani bali ni mchezo wa kirafiki kwa ajili ya kutoa ujumbe
wa amani, na washiriki wa mechi hii wanatoka mataifa mbalimbali na watu wa imani mbalimbali
. Sehemu ya mapato yake yatatengwa kwa ajili ya kufanikisha miradi ya Papa kwa ajili
ya elimu na ustawi wa maisha kwa watu maskini mradi unaofanikishwa na kuendelezwa
na taasisi ya "Scholas Occurentes" ambayo ni taasisi ya elimu, mkono wa Papa Francisko
katika utoaji wa misaada na chama cha "Pupi" kilicho anzishwa na aliyekuwa Argentina
mchezaji wa mpira wa miguu Javier Zanetti na mke wake Paula, kwa ajili udumishaji
juhudi za kutoa msaada katika mradi unaoitwa "maisha mbadala". Kwa ajili hii, pia
unaalikwa kutoa msaada wako katika juhudi hizi kwa kutuma ujumbe wa SMS namba 45593.
Katika
mkutano wa waandishi wa habari, Msgr. Guillermo Javier Karcher, aliwasilisha rasmi
salaam za Papa Francisko, ambamo alitoa shukurani zake za dhati kwa mpango huo uliandaliwa
kwa ajili ya amani, kama alivyowahi kupendekeza siku za nyuma, uwepo wa mechi ya kirafiki
kati ya wachezaji kutoka kila timu na wa dini zote na madhehebu yote Kikristo.Taasisi
ya “Scholas Ocurrentes”, ililichukua kwa makini pendekezo hilo na kuandaa mechi hii
na pia ina lenga kujenga mtandao kwa ajili ya kubadilishana miradi na maadili elimu
kwa ajili ya kuendeleza utamaduni wa mijadala na utamaduni wa amani. Katika mtazamo
huo, Papa Francisko alipendekeza kwamba kabla ya kila mchezo, kila timu ipande mti
wa mzeituni, kama ishara ya amani , kama ilivyo fanyika katika maadhimisho ya mwaka
Mtakatifu 2000, yeye akiwa Askofu Mkuu wa Buenos Aires, alipanda mti katika uwanja
wa Plaza de Mayo , akiwa na wanafunzi elfu saba kutoka shule za Kiserikali bila ya
utengano wa kidini. Waandaaji wa tukio hili wanatumaini, mchezo huu wa kwanza
wa madhehebu,utaweza kuwa hatua ya mwanzo katika juhudi za kueneza ujumbe wa amani
kwa njia ya michezo, kama Papa Francisco alivyo pendekeza. Michezo pamoja na kuwa
ni uwanja wa upinzani kati ya timu mbili zinazocheza, lakini ni tukio ambalo daima
hufanyika katika hali ya amani na utulivu, kuburudisha na kufurahisha mioyo ya watu.
Na hivyo unakuwa ni mfano mzuri wa kuigwa na vyama vya kisiasa , kwamba licha ya kuwa
na maoni tofauti katika utendaji lakini katika utofauti huo, unakuwa ni nafasi ya
kujenga mazuri kwa ajili ya ustawi wa jamii. Na kuwa mchezaji wa mpira au mwana riadha
hakumwondolei mtu imani yake. Imani ni suala linalo ambatana na mtu katika maisha
yake yote. Na ndivyo licha ya watu kuwa na imani mbalimbali, wanapaswa kuchanganyika
na kucheza pamoja kwa amani na utulivu kama ilivyo timu za mpira katika mechi, hucheza
kwa ajili ya manufaa ya wote.