2014-08-27 09:12:34

Kambumbu kuchezwa kwa ajili ya kueneza Ujumbe wa amani duniani


Septemba Mosi katika viwanja vya Olympic vya mjini Roma, kutafanyika mashindano ya mpira wa miguu kati ya timu mbili za kidini kwa heshima ya Papa Francisco, kwa ajili ya kutoa ujumbe wa nguvu wa amani duniani. Ni mpango uliowasilishwa siku ya Jumanne kwa wanahabari katika ukumbi wa Makao Makuu ya Redio Vatican. Kati ya walio shiriki katika mkutano huo ni Msgr. Guillermo Karcher, afisa katika Sekretarieti ya Vatican kwa ajili ya khafla za Kipapa , mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu Javier Zanetti, wakiwepo pia wachezaji kutoka timu ya Lazio, Cristian Ledesma,na Juan Iturbe wa timu ya Roma.

Mchezo huu utakao fanyika katika uwanja wa Olympic Roma, Mosi Septemba 20:45, si mechi za kipinzani bali ni mchezo wa kirafiki kwa ajili ya kutoa ujumbe wa amani, na washiriki wa mechi hii wanatoka mataifa mbalimbali na watu wa imani mbalimbali . Sehemu ya mapato yake yatatengwa kwa ajili ya kufanikisha miradi ya Papa kwa ajili ya elimu na ustawi wa maisha kwa watu maskini mradi unaofanikishwa na kuendelezwa na taasisi ya "Scholas Occurentes" ambayo ni taasisi ya elimu, mkono wa Papa Francisko katika utoaji wa misaada na chama cha "Pupi" kilicho anzishwa na aliyekuwa Argentina mchezaji wa mpira wa miguu Javier Zanetti na mke wake Paula, kwa ajili udumishaji juhudi za kutoa msaada katika mradi unaoitwa "maisha mbadala". Kwa ajili hii, pia unaalikwa kutoa msaada wako katika juhudi hizi kwa kutuma ujumbe wa SMS namba 45593.

Katika mkutano wa waandishi wa habari, Msgr. Guillermo Javier Karcher, aliwasilisha rasmi salaam za Papa Francisko, ambamo alitoa shukurani zake za dhati kwa mpango huo uliandaliwa kwa ajili ya amani, kama alivyowahi kupendekeza siku za nyuma, uwepo wa mechi ya kirafiki kati ya wachezaji kutoka kila timu na wa dini zote na madhehebu yote Kikristo.Taasisi ya “Scholas Ocurrentes”, ililichukua kwa makini pendekezo hilo na kuandaa mechi hii na pia ina lenga kujenga mtandao kwa ajili ya kubadilishana miradi na maadili elimu kwa ajili ya kuendeleza utamaduni wa mijadala na utamaduni wa amani. Katika mtazamo huo, Papa Francisko alipendekeza kwamba kabla ya kila mchezo, kila timu ipande mti wa mzeituni, kama ishara ya amani , kama ilivyo fanyika katika maadhimisho ya mwaka Mtakatifu 2000, yeye akiwa Askofu Mkuu wa Buenos Aires, alipanda mti katika uwanja wa Plaza de Mayo , akiwa na wanafunzi elfu saba kutoka shule za Kiserikali bila ya utengano wa kidini.
Waandaaji wa tukio hili wanatumaini, mchezo huu wa kwanza wa madhehebu,utaweza kuwa hatua ya mwanzo katika juhudi za kueneza ujumbe wa amani kwa njia ya michezo, kama Papa Francisco alivyo pendekeza. Michezo pamoja na kuwa ni uwanja wa upinzani kati ya timu mbili zinazocheza, lakini ni tukio ambalo daima hufanyika katika hali ya amani na utulivu, kuburudisha na kufurahisha mioyo ya watu. Na hivyo unakuwa ni mfano mzuri wa kuigwa na vyama vya kisiasa , kwamba licha ya kuwa na maoni tofauti katika utendaji lakini katika utofauti huo, unakuwa ni nafasi ya kujenga mazuri kwa ajili ya ustawi wa jamii. Na kuwa mchezaji wa mpira au mwana riadha hakumwondolei mtu imani yake. Imani ni suala linalo ambatana na mtu katika maisha yake yote. Na ndivyo licha ya watu kuwa na imani mbalimbali, wanapaswa kuchanganyika na kucheza pamoja kwa amani na utulivu kama ilivyo timu za mpira katika mechi, hucheza kwa ajili ya manufaa ya wote.









All the contents on this site are copyrighted ©.