2014-08-25 16:39:05

Tafakari juu ya siku ya Kukomesha utumwa


Hivi karibuni Mons. Josef Ballong wa Redio Vatican, alitoa tafakari juu ya kumbukumbu ya hati ya kuzuia utumwa duniani. Kumbukumbu inayo fanyika kila tarehe 23.08 ya kila mwaka ambayo ni siku ya kimataifa ya kukumbuka ukomeshaji wa watumwa inayo andaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa UNESCO kwa ajili ya kumbukumbu ya kwanza ya ukomeshaji wa utumwa kwa 1791 huko Santo Domingo. Ni Siku ambayo ni muhimu iliyopelekea kukomeshwa kwa utumwa wa watu weusi.

Katika maelezo yake Padre Ballong alisema kwamba ni siku inayowakilisha majadiliano ya moja kwa moja na kukumbuka kipindi kigumu cha kuhuzunisha katika historia ya kiafrika , kama vile Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili aliwahi kusema kwamba , “ni ukweli haya yalikuwa ni mauaji ya kinyama ambayo kamwe hayatasauhulika.

Lakini watu wa kusahau haswa ni jamii ya waafrika wenyewe, kwasababu ya kutokuwa na mwanga mpana juu ya jamii yao na historia kamili ya kipindi kile cha utumwa na kutokujua kuwa wahusika walikuwa ni waafrika wenyewe.
Aliendelea kueleza kuwa iwapo wanaongelea sana juu ya hati hiyo ya kuzuia na juu ya utumwa wahusika kutoka Ulaya, Marekani, na visiwa vya Caribian , ni dhahili kwamba mara chache wanasahau kuongelea hata matukio haya juu ya ng’ambo ya pili ya sahara.

Pamoja na majadiliano mengi ya kimataifa juu ya tukio hili kama lile la kipindi cha misafara ya utumwa inakuwa vigumu kutambua wahusika wa jamii za kiarabu kwa kipindi cha kale , ya kwamba nao pia ndiyo walikuwa wa mwisho kufanya hati hii na ukomeshaji wa utumwa.
Afrika yenyewe inapaswa kufanya chini juu kwaajili ya viongozi wake na kuwatia moyo vijana ambao ndiyo kizazi kijacho, na kuwahamasisha katika masomo ya kina zaidi yanayolenga, pia kufanya utafiti wa matukio yanayo husu Afrika yenyewe.
Kwa namna hiyo umoja wa Afrika unaweza kuwa ndicho kitu cha msingi , kwasababu ya kuhamasisha kizazi kipya ,hili waweze kupata mafunzo juu ya afrika mpya wawe na utambuzi,na ujuzi wa kuweza kutatua matatizo yanayojitokeza kama vile ubaguzi na ukosefu wa haki.

Tatizo kubwa linalojitokeza lakini ni kile kitendo cha viongozi wa afrika kutojali, na hii ni kwasababu ya kuendelea kujionyesha matukio mbalimbali ya bara hilo.
Matukio hayo ni kama yale yaliyopita na ya kihistoria , yaani ya utumwa, na hata ya sasa kama vile matatizo ya wahamiaji.
Padre anaendelea kutoa maoni yake kuwa hili kuweza kufanikisha jambo hili inahitajika viongozi wa afrika wajihusishe zaidi , na kwa kufanya hivyo inawezekana kabisa kuwa na mwamko katika jamii na hata kutatua matatizo yaliyo makubwa juu ya vijana wa kiafrika kwa ujumla. Ukosefu wa utambuzi kwa ujumla , au ukosefu wa kumbukumbu ya kihistoria katika jamii , inasababisaha mfululizo wa matukio makubwa yanaoneekana.
Anatoa mfano kwamba tazama ni kitu gani kinachojitokeza katika nchi za ulaya ambapo upotezaji wa mila na desturi, ukristo, katika jamiii mbalimbali zimesababisha kukosa muelekeo juu ya hali mpya inayojitokeza.

Anasema kuwa watu wengi wakimbizi kutoka bara la afrika na mashariki ya mbali , inawaopesha jamii ya Ulaya , ambayo daima imekuwa na upungufu wa uzalendo, kwasababu hiyo wanaogopa kukutanan na hali mpya hii ya uhamiaji.

Hii ni kutokana na tabia ya siku nyingi, ambayo matokeo yake ni hasi juu ya matazamo wa wahamiaji wa kizazi cha pili na hasa wale waliozaliwa ndani ya nchi za ulaya, na kuelimishwa katika utamaduni wa kiulaya.
Pia alielezea kwamba udhaifu unaojitokeza katika utambuzi wa dini ya ukristo , umesababisha vijana wengi kutafuta matawi mengine ya hitikadi kali ya kiislam , na kukutana na walimu waongo wa kiroho, na ndipo matukio yamejitokeza ambayo yamepelekea vijana wa ulaya, kuchagua wawe mashahidi wa Jihad , na hata kujiingiza katika vitendo vya kighahidi, kitu ambacho kinachojionyesha katika dunia hii ambamo imejaa wahuaji,haswa kwa kile kinachojionyesha katika macho yao yaani dunia iliyo kosa thamani yake.








All the contents on this site are copyrighted ©.