Kheri za Mlimani ni muhtasari mkuu wa mafundisho msingi yaliyotolewa na Yesu. Hii
ni dira na mwongozo kwa Wakristo. Yesu aliwaachia wafuasi wake amri kuu ya mapendo
kwa Mungu na jirani, mambo yanayopaswa kumwilishwa katika uhalisia wa maisha ya waamini
kila kunapokucha!
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji
wa mitandao ya kijamii anasema kwamba, Kristo ni mtu anayethubutu kutoa kile alichokirimiwa
na Mwenyezi Mungu. Maisha ya Kristo yanapaswa kusheheni matendo makuu ya ukarimu kwa
jirani unaotekelezwa kwa si kwa kupiga matarumbeta, bali katika hali ya usiri, ili
yaonekane na Mwenyezi Mungu ambaye yuko sirini.