Mama Kanisa anatarajia kuadhimisha Sinodi maalum ya Maaskofu kwa ajili ya Familia,
itakayofanyika mjini Vatican kuanzia tarehe 5 hadi tarehe 19 Oktoba, 2014. Mababa
wa Sinodi wataangalia kwa kina na mapana: fursa, changamoto na matatizo yanayozikablia
familia, ili kuwatangazia watu wa mataifa Injili ya Familia ya Kikristo.
Ifuatayo
ni sala inayogusa baadhi ya matatizo na changamoto zinazoendelea kujitokeza katika
familia: Ebu angalia na linganisha na maisha ya familia yako, ili uweze kufanya maboresho
makubwa zaidi katika maisha na utume wa familia.
Ee Mungu wa Upendo na
Amani, tunakuomba utufanye sisi tuwe vyombo vya Amani yako katika Familia zetu kwa
njia ya Sala hii ya Familia Kupendana, kusameheana na kutaabikiana. Na sasa tusali. Penye
Familia yenye CHUKI, tupeleke UPENDO, Penye Familia yenye MAFARAKANO, tupeleke
MAELEWANO Penye Familia yenye MAHANGAIKO, tupeleke UTULIVU Penye Familia yenye
MATESO, tupeleke FARAJA Penye Familia yenye MASHAKA, tupeleke UHAKIKA Penye
Familia yenye UWONGO, tupeleke UKWELI
Penye Familia yenye HUZUNI, tupeleke
FURAHA Penye Familia yenye MAJERAHA, tupeleke UPONYAJI Penye Familia yenye
GIZA, tupeleke MWANGA Penye Familia yenye UKANDAMIZAJI, tupeleke HURUMA Penye
Familia yenye UJINGA, tupeleke ELIMU,HEKIMA NA BUSARA.
Penye Familia yenye
UBINAFSI, tupeleke UKARIMU Penye Familia yenye RUSHWA, tupeleke HAKI Penye
Familia yenye UBAGUZI, tupeleke USAWA Penye Familia yenye UKABILA, tupeleke UDUGU Penye
Familia yenye UFISADI, tupeleke UAMINIFU.
Penye Familia yenye DHARAU, tupeleke
HESHIMA Penye Familia yenye MAJIVUNO, tupeleke UNYENYEKEVU, Penye Familia yenye
MAUAJI, tupeleke UHAI Penye Familia yenye WASIWASI, tupeleke MATUMAINI Penye
Familia yenye UPAGANI, tupeleke INJILI, Penye Familia yenye VIFUNGO, tupeleke
MSAMAHA.
Penye Familia yenye USHIRIKINA, tupeleke UCHAJI Penye Familia
yenye VURUGU, tupeleke AMANI, Penye Familia yenye UADUI, tepeleke URAFIKI.
Ee
Mungu uzifanye familia zetu ziige mfano wa Familia yako Takatifu ya Nazareti, ya Yesu,
Maria na Yosefu. Amina!
Bikira Maria Malkia wa Familia, utuombee! Mtakatifu
Yosefu Mlinzi wa Familia zetu, utuombee! Mtakatifu Yosefu Kitisho cha mashetani,
utuombee! Mtakatifu Yosefu uzuri wa mwenendo wa nyumbani, utuobee! Moyo wa Yesu
chemchemi ya uzima, utakatifu na faraja zote, Utuhurumie!