2014-08-16 11:44:24

Hotuba ya shukurani kutoka kwa Kardinali Andrea Yeum Soo-jung



Baada ya Maadhimisho ya Ibada ya Misa Takatifu Kardinali Andrew Yeoum Soo Jung, alitoa hotuba ya shukurani kwa Papa Francisko, ambaye ameonyesha upendo mkuu kwa taifa la Korea. Alisema, Baba Mtakatifu, kwa niaba ya watu wote wa Korea, walei pamoja watawa na viongozi wa dini wa kanisa zima la Korea, kwa mara ingine ninakukaribisha kwa furaha kuu.

Kardinali alirejea historia kwa ufupi akisema, Kanisa Katoliki Korea tayari lina watakatifu 103 na mashahidi wafia dini 124, kwa kuongeza ulio watangazwa leo kuwa Wenye heri. Na kwamba, eneo hili kuzunguka Gwanghwamun, imekuwa ni kitivo cha historia kutokana na wahenga waamini wengi, kuwa mashahidi wafia dini wa imani Katoliki.

Kardinali aliendelea kueleza kwamba Kanisa Katoliki Korea, kwa damu waamini mashahidi wafia dini iliyomwangika, imethibitisha kuwa mfano mzuri wa kuigwa na jamii yote ya Korea katika kukuza unyofu wa moyo na haki za binadamu. Na Hivyo, Kardinali alionyesha tumaini lake kwamba , maadhimisho ya Ibada ya kuwataja wenye heri iliyokamilika limekuwa ni tukio linalo dai kujenga amani na umoja wa Wakatoliki si tu Korea lakini Pia watu wa Korea na jamii yote ya watu wa Asia, kupitia utandawazi wa udugu.

Kardinali alimhakikishia Papa kwamba, Kanisa la Korea siku zote, hujitahidi kuwa mwanga na chumvi ya Uinjilishaji duniani na katika kuwa mhudumu wa maskini, wateswa, waliotengwa, kwa kuwafariji kwa furaha ya Injili. Kardinali Soo-jung alikamilisha hotuba yake kwa kuomba baraka za Papa kwa Kanisa nchini Korea.








All the contents on this site are copyrighted ©.