2014-08-14 11:55:15

Shirika limekuwa na kuchanua, matunda yanaanza kuonekana!


Miaka ishirini na mitano ya Shirika la Masista wa Pendo la Huruma wa Mtakatifu Vinsenti wa Paulo, Mitundu - Singida ni kielelezo cha huruma na upendo wa Mungu kwa ajili ya ustawi na ukuaji wa Kanisa nchini Tanzania, hususan eneo la Mitundu ambalo kwa wengi lilidhaniwa kuwa ni pembezoni mwa jamii, lakini huko ndiko ambako Shirika limejikita na sasa matunda yake yanaanza kuonekana kwa kusherehekea Jubilee ya Miaka 25 ya uwepo wao nchini Tanzania.

Tunaposherehekea tukio kubwa la kihistoria katika Shirika letu, yaani Jubilei ya miaka 25 tangu kuanzishwa Shirika hapa Mitundu – Tanzania, kama familia ya kivinsenti tunaalikwa kumwinulia Mungu Mtakatifu mioyo yetu na kusema asante kwa makuu aliyotutendea.

Ufalme wa Mungu umefanana na punje ya haradali nayo ni ndogo kuliko mbegu zote lakini ikiisha kumea huwa kubwa kuliko mimea yote hata ndege wa angani huja na kujenga viota katika matawi yake (Mt.13:31-32).

Hivyo tunapotafakari matendo makuu aliyotutendea Mungu tumeona ni vema tutafakari na kutembea katika Maandiko haya Matakatifu, tukiyafananisha na ukuaji wa Shirika letu hatua kwa hatua ndani ya Maongozi ya Mungu.

„Maongozi ya Mungu yametuleta hapa“ (maneno ya Mtakatifu Vinsenti wa Paulo).Waasisi wetu waliisikia sauti ya Mungu na katika fumbo Mungu alifunua mpango wake kwa:

Katika hayo yote Mungu alitaka kuonesha ukuu wake na uwezo wake: „Kwa subira yenu mtayaokoa maisha yenu “(Mk 13:13). Na Mtakatifu Vinsenti wa Paulo anasema: „Uvumilivu kidogo na tazama yamepita“.

Mungu kwa wema na upendo wake akayahuisha matumaini ya mche kwa kuupa ustawi tena. Hapa tunayatafakari maneno ya hekima ya Mt. Vinsenti yasemayo: „Tunahitaji neema kwa kuanza lakini zaidi kwa kudumu“


Mungu upokee sifa na shukrani kwa baraka na neema zako maridhawa ulizoutendea mtii huu ambao unazaa matunda yanayogawanywa kwa maskini.
Katika Mwaka huu wa Jubilei tutembee hatua kwa hatua tukialikwa kuyapokea maisha ya wito, kuyaendeleza na kuyapa sura stahiki.Tunatumwa katika yote kumpa Mungu kipaumbele na Injili ya Mwanaye na kuwafanya wanadamu na hasa maskini wakutane na Pendo la Huruma.
Mungu libariki Shirika letu.
Mungu wabariki waasisi wetu.
Mungu tubariki sisi sote.








All the contents on this site are copyrighted ©.