Baba Mtakatifu Francisko amemwandikia ujumbe Askofu mkuu Giovanni Paolo Benotto wa
Jimbo kuu la Pisa, Kaskazini mwa Italia, katika kumbu kumbu ya miaka sabini, tangu
watu 560, kati yao wakiwemo Mapadre wawili walipouwawa, huko Stazzema, Toscana na
Vikosi vya Kinazi, tarehe 12 Agosti 1944.
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe
huu ambao umeandikwa kwa niaba yake na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican
anamwomba, Yesu Mfalme wa amani, awawezeshe Watu wa Mataifa kujikita katika amani
na utulivu. Anaendelea kuwakumbuka na kuwaombea watu wote walioathirika kutokana na
mashambulizi haya. Anawaweka wote chini ya ulinzi na faraja kutoka kwa Bikira Maria.