Wakati huu ambapo hatima ya Wakristo nchini Iraq iko mashakani kutokana na mashambulizi
na madhulumu wanayofanyiwa, Baba Mtakatifu Francisko anawaalika waamini na watu wpte
wenye mapenzi mema kujiunga pamoja naye, ili kusali kwa ajili ya kuwaombea Wakristo
nchini Iraq na Jumuiya za Kikristo ambazo kwa sasa zinakabiliana na madhulumu ya kidini!
Baba
Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake wa pili, Ijumaa tarehe 8 Agosti 2014 kwa watumiaji
wa mitandao ya kijamii, anawaalika kwa mara nyingine tena waamini pamoja na watu wote
wenye mapenzi mema kutenga muda kidogo kwa ajili ya kusali kwa watu wote nchini Iraq
ambao wanalazimika kuyakimbia makazi yao kutokana na vurugu za kidini.