2014-08-07 16:16:55

Mshikamano wa Papa na wananchi wa China waliokumbwa na tetemeko la ardhi!


Baba Mtakatifu Francisko mara baada ya Katekesi yake kwa mahujaji na wageni waliokuwa wamefurika mjini Vatican, Jumatano tarehe 7 Agosti, 2014, amewakumbuka na kuonesha mshikamano wake wa pekee kwa wananchi wa China waliokumbwa na tetemeko la ardhi ambalo hadi sasa limekwishasababisha maafa makubwa.

Taarifa zilizotolewa na Serikali, Alhamisi tarehe 7 Agosti 2014 zinaonesha kwamba, watu 589 wamefariki dunia, watu 9 hawajulikani mahali waliko na wengine 2, 401 wamepata majeraha makubwa. Serikali ya China imelazimika kuwahamisha wananchi 230, 000 kutoka katika makazi yao, ili kuwapatia hifadhi mahali pa salama zaidi.

Baba Mtakatifu anawaombea marehemu waliopoteza maisha yao kwenye Jimbo la Yunnan na anawakumbuka katika sala zake, wote waliokumbwa na janga hili. Baba Mtakatifu katika tafakari yake kwa lugha ya kiarabu amewakumbuka na kuwaombea pia wananchi wa Iraq ambao kwa sasa wanateseka kutokana na vita kupamba moto hasa eneo la Kaskazini mwa Iraq. Anawaombea ili amani ya kweli iweze kupatikana!







All the contents on this site are copyrighted ©.