2014-08-07 12:13:09

Familia inapaswa kutawaliwa na maneno matatu, samahani, Asante na tafadhali- Papa


Baba Mtakatifu Francisco, amepeleka ujumbe kwa Kongamano la Kimataifa la Amerika ya Kusini linalojadili masuala ya familia. Kongamano hili limeandaliwa na Baraza linalounganisha Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Amerika ya Kusini (CELAM), chini ya mada kuu: Familia na Maendeleo ya Kijamii kwa ajili ya ukamilifu wa Maisha na umoja wa katika utume. Kongamano hili la siku tano 4-9 Agosti, majadiliano yake yanalenga kutoa mchango katika Sinodi maalum juu ya Familia, itakayofanyika Vatican mwezi Oktoba 2014.

Ujumbe wa Baba Mtakatifu unatoa mchango katika swali linalouliza: familia ni nini? Anasema, licha ya matatizo yake makubwa, na mahitaji yake ya kidharura, familia ni kiini cha upendo,wenye kutawaliwa na sheria ya kuheshimiana na kushikamana na uwezo wa kuhimili mashambulizi ya kudanganywa na utawala wa nguvu za dunia. Katika miali upendo wa nyumbani, mtu huwa na hisia kali za kutambua yeye ni mmoja wa wanafamilia katika asili yake ya usawa katika kundi binadamu, na hivyo hukabiliana na upinzani potofu wa uongo kati ya mtu binafsi na jamii.Katika asili yake, ndani ya familia, hakuna hata mmoja anayetegwa: watoto na mzee hupokelewa na mna utamaduni wa kukutana na kuzungumza kwa uwazi katika hali za mshikamano na huduma zake kwa makuzi ya watoto.


Na hivyo Papa anasema, familia ina thamani kubwa, ni hazina na utajiri wa jamii, (kama alivyoandika Papa Benedikto XVI, katika waraka wake wa Upendo katika Ukweli , 44). Kwa maana hiyo, alipenda kusisitiza mambo mawili muhimu katika mchango wake, nayo ni msingi wa : utulivu na uzazi.


Baba Mtakatifu Francisco , kwanza ametaja misingi ya uaminifu katika ndoa hata mpaka kufa, na ndivyo ilivyo kwa familia hujifunza maisha ya ndoa, maana ya kuwa mzazi na kuwa ndugu na kuishi ndani ya kaya moja . Mahusiano haya huunda msingi wa jamii ya binadamu, katika mshikamano, usawa na akili ya kujisikia kuwa sehemu ya watu, kujisikia karibu, na kujali waliobali mbali zaidi na au wale ambao kimaisha hawakubahatika. Majiundo haya ya moyo wa ubinadamu katika mahusiano na wengine, hujenga usalama msingi kwa mtu kuwa tayari kuhudumia wengine
.

Baba Mtakatifu anaendelea kueleza kwamba, upendo wa familia ni matunda mazuri si tu kwa sababu huzaa maisha mapya, lakini pia kwa sababu hukuza upeo wa macho katika uwepo wake , na ujenzi wa ulimwengu mpya,. Inafaa binadamu kuamini hilo, na kukata tamaa hila zote za kutaka kushindwa kutimiza misingi ya familia , hasa mshikamano misingi, heshima na uaminifu. Papa aliendelea kuangalisha katika hatari za kidunia zinazokabili familia, na hasa kupenda mali za dunia kupindukia, hata kupunguza umuhimu wa familia katika misingi yake ya kupanuka na kutumikia.


Hatimaye, Baba Mtakatifu alitoa shukurani zake za dhati kwa uwepo wa uzoefu huu uliosimikwa katika misingi ya familia , ambamo binadamu hukua katika uwazi wa kumwona Mungu kama Baba. Kwa hili, waraka wa Aparecida, pia unaonyesha kwamba, familia ni lazima kuchukuliwa si tu kama chombo cha uinjilishaji, lakini pia kama wakala wa uinjilishaji (432 cf. nn., 435), ambamo ndani mwake, tunaweza kuitafakari sura ya Mungu ,katika fumbo lake kamili, kama familia na kwa namna hiyo , tunapata kuona upendo wa kibinadamu kama ishara ya upendo wa Mungu na uwepo wake (Lumen fidei, 52). Katika familia, imani na upendo huchanganywa na maziwa ya mama. Papa Francisco ameeleza na kutaja mazoea ya famlia kuomba kwa hiari baraka kama inavyofanywa na wengi , ni mfano halisi wa uongofu wa kibiblia kwamba baraka za Mungu, hupitishwa kutoka kwa baba hadi kwa wana.


Kufahamu kwamba upendo familia una thamani kubwa, na kwamba kila tendo la binadamu linapaswa kuongeza thamani ya familia, na hivyo, ni muhimu kuhamasisha familia kujenga uhusiano mzuri miongoni mwa wanachama wake, kujua jinsi ya kusema kwa kila mmoja, bila kupoteza maneno makuu matatu: Nisamehe, Asante, na tafadhali, na kumgeukia Mungu, Jina nzuri la Baba wa Mbinguni


Papa Francisco amemalizia ujumbe wake kwa kuomba Msaada wa Mama yetu ya Guadalupe awezeshe kutoa baraka tele za Mungu kwa ajili ya familia za Marekani na katika kuzaa mbegu za maisha yenye maelewano na imani thabiti yenye kulishwa kwa Injili na matendo mema. Papa pia amewaomba wasisahau kuomba kwa ajili yake, maana anahitaji maombezi yao. .







All the contents on this site are copyrighted ©.