Vyama vyote Msumbiji, ruksa kushiriki uchaguzi mkuu!
Tume huru ya uchaguzi nchini Msumbiji imetangaza kwamba, hakuna chama chochote cha
kisiasa nchini humo ambacho kinazuiliwa kushiriki kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika hivi karibuni nchini Msumbiji. Hii ni hatua muhimu sana katika mchakato
wa kutaka kulinda, kujenga na kudumisha misingi ya haki, amani na demokrasia ya kweli.
Msumbiji inatarajiwa kufanya uchaguzi mkuu mwezi Oktoba, 2014.
Tangu mwaka
2013 Msumbiji ilijikuta ikiingia tena kwenye kinzani na migogoro ya kijamii iliyopelekea
wasi wasi wa kuzuka tena kwa vita ya wenyewe kwa wenyewe, pale ambapo Chama cha Upinzani
cha RENAMO kilipoamua kupimana nguvu na Majeshi ya ulinzi na usalama ya Serikali ya
Msumbiji. Katika kujenga mahusiano ya amani na utulivu, RENAMO na FRELIMO wamehitimisha
kuratibu mambo msingi yatakayoingizwa kwenye waraka wa utekelezaji wa amani na utulivu
nchini Msumbiji.