Kuna baadhi ya watu wanadhani kwamba, furaha ya kweli inapatikana kutokana na wingi
wa mali ambayo mtu amejikusanyia katika maisha yake. Kwa wengine, furaha hii inajikita
kwa kuwa na mamlaka pamoja na madaraka hata kama mambo haya yanapatikana kwa kwa kupindisha
sheria na kanuni maadili. Hatari ya tatu ni sifa ambazo mtu anazitafuta kwa nguvu
mara baada ya kujipatia mali na madaraka.
Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe
wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii anasema kwamba, ukijilimbikizia utajiri
kama hazina ya maisha yako, utapoteza roho yako!