2014-08-04 09:58:26

Tanzia: Kardinali Edward Clancy amefariki dunia.


Tunasikitika kutangaza kifo cha Kardinali Edward Beda Clancy, Askofu Mkuu Mstaafu wa Sydney, kilichotokea Jumapili iliyopita, 3 Agosti 2014, kama ilivyotangazwa na Ofisi ya Mjumbe wa Papa Australia .

Kardinali Edward Beda Clancy, amefariki akiwa na umri wa miaka 90. Alifanywa kuwa Kardinali na Papa Yohana Paulo II katika kikao cha Makardinali cha Juni 28, 1988. Alijiuzuru kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Sydney Machi 26, 2001.

Kwa Kifo cha Kardinali Clancy , Dekania ya Makardinali sasa imebaki na Makardinali 211 Makardinali, ambao 118 ni wapiga kura na 93 si wapiga kura.

Marehemu Askofu Mkuu Mstaafu Edward Beda Clancy wa Sydney, alizaliwa Desemba 13, 1923 Lithgow, katika Jimbo la Bathurst. Baada ya kumaliza masomo yake katika shule katika Richmond na Santa Monica, alijiunga na Chuo cha Mapadre Maria( Marist) cha Parramatta. Alipadrishwa Julai 23, 1949 na Kardinali Gilroy Na mwaka 1952 alipelekwa Roma kuendelea na masomo katika Chuo cha Mtakatifu Petro , ambako alifuzu katika teolojia na Maandiko Matakatifu katika Taasisi ya Kipapa ya Biblia , katika Chuo Kikuu cha Urbaniana. 1955 - alirudi Australia na kuhudumu katika parokia ya Elizabeth Bay na Liverpool. Nel Februari 1958 aliteuliwa kuwa Profesa wa Maandiko Matakatifu katika Chuo cha Mtakatifu Columba cha Sprinfield. Na aliteuliwa kuwa Kasisi katika Chuo Kikuu cha Sydyney na Profesa wa Maandiko Matakatifu katika Chuo cha Mtakatifu Patrick cha Manly. Oktoba 25, 1973 aliteuliwa kuwa Askofu wa Jina wa Kanisa la Ardi Carna na baadaye kufanya Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu la Sydney, na kuwekwa wakfu wa Askofu Januari 19, 1974, Katika ibada iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa Sydney, Kardinali Freeman.

Na Novemba 24, 1978 alifanywa kuwa Askofu Mkuu waJimbo Kuu la Canberra. Mwaka 1983, Papa Yohana Paulo 11 alimteua kuwa Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Sydney. Na 28 Juni 1988,alifanyw akuwa Kardinali . Aliongoza Jimbo Kuu la Sydney hadi Machi 2001, alipostaafu kwa mujibu wa umri. Pamoja na nyadhifa nyingine za kitume , kati ya 1986 na 2000, alikuwa Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki la Australia . Na pia akiwa Mjumbe wa Kamati ya Kimataifa ya Kiingereza katika Liturujia. Ni aliwahi kuwa Naibu Mwenyekiti wa tisa, wa Mkutano Mkuu wa Sinodi ya Maaskofu wa 1994, juu ya maisha yaliyowekwa wakfu.
Mungu amlaze pema peponi.








All the contents on this site are copyrighted ©.