Papa atoa msamaha kwa Padre Brockmann, kuadhimisha tena Fumbo la Ekaristi Takatifu!
Baba Mtakatifu Francisko ametoa msamaha kwa Padre Miguel D'Escoto Brockmann, mwenye
umri wa miaka 81kutoka Shirika la Wamissionari wa Maryknoll aliyekuwa amesimamishwa
kutoa huduma za Kipadre kutokana na kujihusisha na masuala ya kisiasa.
Adhabu
hii ilitolewa kwenye miaka 1980 na wakati wote huu Padre Brockmann amekuwa akitumikia
adhabu hii kutokana na kujihusisha kwake na masuala ya kisiasa nchini Nicaragua, ingawa
tangu wakati huo aliendelea kubaki mwaminifu kwa Shirika lake la Myarknoll. Kwa miaka
kadhaa sasa Padre Brockmann alikuwa maeachana na masuala ya kisiasa. Hivi karibuni
ameamua kwa utashi wake mwenyewe kumwandikia barua Baba Mtakatifu Francisko akiomba
huruma ili aweze kuadhimisha tena Fumbo la Ekaristi Takatifu kabla ya kuitupa mkono
dunia, ombi ambalo limeridhiwa na Baba Mtakatifu Francisko!
Baba Mtakatifu
ametoa maagizo kwa mkuu wa Shirika la Wamissionari wa Maryknoll kumsaidia ndugu yake
katika Kristo katika mchakato wa kurudi tena katika maisha na utume wa Kanisa kama
Padre Mkalatoliki.