Baba Mtakatifu Francisko amesikitishwa kwa taarifa ya ajali ya ndege iliyotokea Alhamisi,
tarehe 24 Julai 2014, Kaskazini mwa nchi ya Mali, ikiwa na abiria 118 na kuanguka
baada ya kuwa imekwisharuka kwa takribani dakika 50. Abiria wote waliokuwa kwenye
ndege hii kutoka nchini Hispania kwenye Kampuni ya Swiftair na kukodiwa na Shirika
la ndege la Algeria, Air Algerie. Ndege hii ilikuwa inasafiri kutoka Ouagadougou,
Burkina Faso kuelekea Algeri, nchini Algeria.
Katika ujumbe uliondikwa kwa
niaba yake na Kardinali Pietro Parolin, Katibu mkuu wa Vatican kwenda kwa Askofu mkuu
Ghaleb Bader wa Jimbo kuu la Algeria, Baba Mtakatifu anaungana na watu wote waliofikwa
na msiba huu mzito na anawaombea kwa Mwenyezi Mungu, ili aweze kuwapatia raha ya milele
marehemi wote waliopoteza maisha yao kwenye ajali hii. Anawaombea faraja wote walioguswa
na msiba huu!