2014-07-21 14:54:22

Rais wa CRS asema, wataendelea kusaidia AMECEA


Shirika la Misaada Katoliki (CRS) limeahidi kuendeleza msaada wake kwa AMECEA, kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa mkakati iliyokubalika kutoa jibu, kwa Waraka wa Kitume uliotolewa na Papa Benedikto XVI, baada ya sinodi Maalum ya Maaskofu kanda ya Bara la Afrika, Waraka wenye jina "Dhamana ya Afrika “ (Africae Munus)”.

Akizungumza katika kikao cha 18 cha AMECEA, Jumamosi iliyopita, Julai 19, 2014, Rais na Afisa Mtendaji Mtendaji Mkuu wa Ofisi (CEO) ya CRS, Dk Carolyn Woo aliirejea mandhari iliyofungua Mkutano huo, "Uinjilishaji Mpya, kupitia njia ya Wogofu na kushuhudia Imani ya Kikristo, kwamba, ni mada makini kwa CRS. "Kutoa ushuhuda wa imani yetu, hasa miongoni mwa watu wenye shida na waliotengwa na jamii , ni kiini cha utendaji wote wa shirika hilo la CRS, na mkakati wa shirika katika kuimarisha ushirikiano wake na wanachama AMECEA, katika mshikamano wa kutoa huduma kwa maskini na wanaoishi katika mazingira magumu".
Dk Woo alieleza jinsi wafanyakazi wa CRS, walivyo tayari kushirikiana na AMECEA kutathmini yale yaliyokwisha fanikishwa na kile ambacho bado kinahitaji msukumo nangvu zaidi, tangu kutolewa kwa AfricaeMunus, na katika mtazamo mpya wa Mipango Mbinu, katika mkakati wa maendeleo ya AMECEA. Na hivyo CRS, inatarajia kujifunza zaidi juu ya mpango mpya wa miaka 10, kiufundi, vifaa na msaada wa fedha unaohitaji sasa, ikilinganishwa na siku za nyuma.

Rais alisema, CRS inatambua changamoto zinazopambanisha watu katika mkoa AMECEA, ikiwemo migogoro ya ndani na baina ya mataifa, pia yenye kuvuka mipaka ya kidini, hali ya hewa, uhaba wa chakula, ajira kwa vijana, na biashara ya binadamu nk

Padre Chrsisantus Ndaga, Katibu wa Kitengo cha Mawasiliano cha AMECEA, anaripoti zaidi kwamba, Rais wa CRS, imeonya wanachama wa AMECEA kwamba, iwapo matatizo hayo yatabaki bila kupatiwa ufumbuzi, vitisho hivi vinaweza kwa haraka kubadili mafanikio yaliyopatikana hadi sasa. Na kwa bahati CRS, imekuwa ikisaidia utekelezaji wa miradi mingi katika ngazi za kijimbo katika kanda AMECEA. Na kwamba CRS, itaendelea na ushirikiano na kusindikizana katika roho ya Papa Benedict XVI, aliyoionyesha katika barua yake binafsi, juu ya Fadhila, na Azimio la 2012 la Kinshasa la Maaskofu wa Afrika.








All the contents on this site are copyrighted ©.