Papa kutembelea mjini Caserta, hapo tarehe 26 Julai 2014
Katika maadhimisho ya kumbu kumbu ya watakatifu Joakim na Anna, wazazi wake Bikira
Maria, inayoadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 26 Julai, Baba Mtakatifu Francisko
anatarajiwa kutembelea mji wa Caserta, ulioko mkoani Campania.
Saa 12:00 Jioni,
Baba Mtakatifu anatarajiwa kukutana na Makleri na hatimaye, kuadhimisha Ibada ya Misa
Takatifu kwa ajili ya waamini wa Caserta kwani Mtakatifu Anna ni msimamizi wa mji
huu.
Ufafanuzi huu umetolewa na Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican
na kwamba, Baba Mtakatifu Francisko atarejea tena mjini hapo Jumatatu tarehe 28 Julai
2014 ili kumtembelea rafiki yake Giovanni Traettino, mchungaji wa Kanisa la Kiinjilisti.