2014-07-12 15:55:51

Jumapili ni siku ya mabaharia na wavuvi


Jumapili hii ni Siku ya watu wanaoishi na kufanya kazi katika maeneo ya bahari. Kwa ajili hiyo, Kardinali Antonio Maria VegliĆ², Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya wakimbizi, wahamiaji na Watu wanaohamahama, akihojiwa na Mwanahabari Mario Ponzi , amesema pamoja na kero nyingi zinazofanyika katika ulimwengu wa bahari, hakuna hata mmoja anayeweza kutengwa katika Kazi za kichungaji za Kanisa. Alitaja baadhi keoro zinazosumbua kuwa ni uharamia kwa usafiri wa watu na bidhaa majini, kukataliwa kwa makazi ya Wagypsy, utalii kama injini ya maendeleo ya binadamu, pamoja na mengine yanayofanyika katika ulimwengu huu wa Bahari.

Na Kardinali Veglio, alieleza kuwa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kazi za Kichungaji kwa Wakimbizi , watalii na watu wasiokuwa na makazi maalum kama Mabaharia na wavuvi katika Ulimwengu wa Bahari, kwa njia ya mikutano ya kimataifa, na upelekaji wa ujumbe wake na ufadhili , linaendelea kuzingatia tahadhari ya dunia juu ya mambo haya yanayoathiri watu.

Pamoja na kuzungumzia watu wa bahari, lakini pia mawazo yake aliyapeleka kwa watu wanaoishi mitaani , na pia juu ya wa siku kujitolea na siku ya utalii, katika nyanja chanya na hasi. Na kwamba . ulimwengu wa mabaharia, kwa wengi haujulikani ingawa kuna kundi kubwa la binadamu wapatao zaidi ya milioni moja wanaoishi katika ulimwengu wa maji, wakiwemo mamia ya maelfu ya Mabaharia na Manahodha wa meli wanaosafiri kila siku katika ulimwengu wa bahari. Hivo Kanisa haliwezi kupuuza dunia hii inayoishi mbali na upeo wa macho ya wanaoishi nchi kavu au kupuuzwa na jamii kwa ujumla, wakati wakipita katika bandarini.

Madhumuni ya kuwa na Siku ya ulimwengu wa Bahari ambayo hufanyika kila mwaka 13 Julai, katika mzunguko wa Kanisa Katoliki, lakini pia kwa madhehebu mengine ya kikristo, ni kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kazi iliyofanywa na inayoendelea kufanywa na mabaharia katika maisha ya binadamu kila siku. Kardinali amelitaja hili kuwa ni deni kwa watu wanaoishi nchi kavu, kwa sababu hutegemea mengi kutoka sekta ya bahari, ikiwemo usambazaji wa chakula na bidhaa kwa ajili ya matumizi yetu ya kila siku.

Kardinali Veglia pia alirejea hatari zinazokabili taaluma ya duniani hii, na kukiri kwamba, kuna matatizo mengi na hatari mbele ya uso wao kila siku, na hata kama inaonekana, na hasa hatari inayoonekana kuwa kubwa leo hii ni uharamia, kama taarifa zinavyosikika toka hapa na pale, hasa utekwaji nyra wa vyombo vya majini kwa madai ya kulipwa fidia kama ilivyosikika katika bahari ya Ghuba ya Aden. Ingawa sasa katika eneo hilo, tatizo limepungua baada ya kuwepo walinzi wenye silaha kali lakini bado hapajawa salama kabisa.


Katika miezi ya karibuni kumeanza tena baadhi kumekuwa na vurugu katika Ghuba ya Guinea, na katika ukanda wa Malacca na katika bandari nyingi za Amerika ya Kusini. Katika hili , utume wa Kanisa kwa wakazi wa Bahari hutoa ujumbe wa amani na matumaini katika nguvu ya Mungu na majitolea ya nguvu ya mshikamano katika utoaji wa msaada wa kiroho si tu kwa waathirika wa uharamia baharini , lakini pia kwa familia zao, kuwafariji katika yote maumivu ya kisaikolojia na kiroho na matokeo yake.








All the contents on this site are copyrighted ©.