2014-07-12 16:13:59

Dunia kuelekea uchumi shirikishi


Tangu Ijumaa katika ukumbi wa Casina Pio IV,wa hapa Vatican , kumekuwa na warsha ya Kimataifa ya siku mbili 11-12 Julai , iliofanyika katika mazingira ya faragha, kama ilivyoandaliwa na Baraza la Kipapa a Haki na Amani na Sekretarieti ya Nchi, juu ya haki katika manufaa ya dunia, kuelekea uchumi shirikishi katika ngazi ya kimataifa na mshikamano wenye umoja zaidi ,katika uchumi .

Mkutano ulihudhuriwa na wasomi Sabini, wawakilishi wa biashara kubwa na vyama vya kiraia, kama ilivyoandaliwa na kupangwa kwa kushirikiana na taasisi za kimataifa, ikiwemo Benki ya Dunia, Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi Maendeleo (OECD / OSCE), Mkutano wa Umoja wa Mataifa juu ya Biashara na Maendeleo (UNCTAD),na mashirika mengine IMF, FAO, ILO. Madhumuni ya mkutano ni kuimarisha mtazamo uliotajwa na Papa Francisco, katika waraka wake wa Kitume, wenye jina “Evangelii Gaudium"Furaha ya Injili : kwamba ni muhimu daima mipango ya uchumi kuwashirikisha wote.

Majumuisho ya agenda za majadiliano yanaelezea semina, hasa ililenga kuchambua maelezo msingi ya Papa Francisco katika waraka wake wa Injili ya Furaha, katika masuala ya uchumi, ambamo ametaja misingi ya kuheshimu utu wa binadamu na uungaji mkono juhudi zote zinazolenga kutetea haki na uvumilivu ili kwamba, hakuna uchumi wa kutengana. Ni kuondokana na hali ya sasa ambamo binadamu anachukuliwa kama ni bidhaa za kutumika na kutupwa!. Papa ameonya kwamba kizazi cha leo, kimetengeneza utamaduni wa kutupa , ulioenea kote. Si tena suala jepesi la uwepo wa unyonyaji na ugandamizaji, lakini mfumo mpya wa aina yake.

Waraka unaendelea kuonya dhidi ya utengano wa kimbinu katika mifumo muhimu ya maisha ya kijamii, ambamo kila njia ya kujiinua kwa watu maskini, imezibwa kiujanja na wale waliotangulia na, na hivyo hakuna tena sehemu Maskini wanapoweza kujiinua isipokuwa kwa huruma ya mabwanyenyena mabepari .

Pamoja na onyo hilo, Papa hakusahau kuwataja wale wanaofanya vyema, baadhi ya viongozi wa makampuni makubwa na wafanya biashara, ambao hutoa mchango mkubwa fedha na majitoleo binafsi kwa ajili ya kufanikisha maendeleo ya binadamu katika karne hii. Na Papa anataja uwepo wa baadhi ya viongozi wa uchumi duniani wanaoonyesha nia na ubunifu kwa ajili ya kuboresha maisha ya watu wengi katika na ukweli wao kama watalaam .

Hivyo kupitia semina hii , Baba Mtakatifu alitegemea washiriki watachambua kwa kina jinsi gani uchumi unaweza kupanua faida zake na kupunguza matundu mabaya na hali mbaya za uchumi. Kama alivyosema mapema mwaka huu ,Fedha na biashara ya kimataifa inaweza kuchangia zaidi katika uwekezaji wa ujuzi kwenye huduma ya walio badokatika hali mbaya ya umasikini.
Hivyo Semina ililenga kujadili mambo haya na kupendekeza njia zinazoweza kufaa zaidi katika kuinua ukuaji wa uchumi kwa watu wote .
Hivyo kwa njia ya semina hii, Baraza la Kipapa kwa ajili ya haki na amani,, nalo linategemea kupata ufahamu wa ziada na msaada katika kuelewa vizuri zaidi jinsi ya kuboresha mambo mengi ya binadamu ndani ya uchumi wa utandawazi na kuwezesha watu wanaokadiriwa kufikia milioni mbili kutoka katika umaskini wa kukithiri.









All the contents on this site are copyrighted ©.