Papa Francisko ataka mabadiliko ya haraka katika Idara ya uchumi Vatican
Kardinali George Pell, Mkuu wa Sekretarieti ya Uchumi ya Jimbo Takatifu, anasema
, kuna changamoto nyingi na kazi nyingi za kufanya kwa ajili ya ufanikishaji wa mabadiliko
katika Idara ya Uchumi ya Jimbo Takatifu, hilo alilieleza, Jumatano asubuhi , wakati
akikutana na wanahabari katika Ofisi za Vatican, baada ya Taasisi ya Fedha ya Vatican
kutoa taarifa yake. Kardinali alitangaza jitihada kubwa zinazo takiwa kushughulikiwa
kwa haraka, katika sekta ya APSA (Utawala wa urithi mali za Jimbo la Papa, ), Mfuko
wa Pensheni, Mawasiliano na IOR (Taassi ya Benki ), chini ya Uongozi wa Rais mpya
Jean -Baptiste de Franssu.
Katika Mkutano huu wa wanabahari , Rais wa IOR
aliyemaliza muda wake, , Ernst von Freyberg, aliwaambia wanahabri kwamba, Papa Francisco
anapenda kuona mabadiliko ya haraka. Na Kardinali Pell, ameahidi kushughulikia
mapungufu na mianya ya hatari katika kuvujisha fedha , iliyotajwa na Tume ya Kipapa,
iliyofanya utafiti na kushughulikiwa shirika kiuchumi la utawala wa Kiti Kitakatifu
Cosea). Kwa ajili hii, iliundwa Ofisi ya Usimamizi, iliyoongozwa na Danny Casey
raia wa Australia Meneja wa zamani wa Biashara jimbo Kuu la Sydney.
Kwa ajili
ya mambo ya kawaida kwa urithi wa mali ya Vatican (APSA) inayohamishika ,Jumatano
kulichapishwa barua Binafsi “ Motu Proprio ya Papa, inayoamrisha Sekretarieti ya
Uchumi, kusimamia mashirika ya Jimbo la Papa, sera na taratibu kwa ajili ya ununuzi
na usambazaji wa rasilimali watu. Wafanyakazi wa APSA, watashughulikia zaidi masuala
ya hazina, uimarishaji na uanzishaji wa uhusiano wa karibu na benki kuu zote kuu
- kama inavyotakiwa na MONEYVAL - kuhakikisha utulivu wa fedha na ulipaji wa madeni
kwa Jimbo Takatifu.
Kuhusu Mfuko wa Pensheni, imeteuliwa kamati ya watalaam
wakiongozwa na Monsinyori Brian Ferme, akisaidiwa na wajumbe wanne wataalam Kotanko
Bernhard (Austria), Andrea Lesca (Italia), Antoine de Salins (France), Prof. Nino
Savelli (Italia) kulingana na muundo wa marekebisho yaliyo pendekezwa katika kwa
Baraza la Uchumi 2014 kw alengo la kuhakikisha pensheni kwa sasa na kizazi kijacho
ni salama zaidi.
Pia kutakuwa na marekebisho katika Idara ya Mawasiliano Vatican,
kulingana na mwenendo mpya wa matumizi, na uboreshaji wa uratibu na kupunguza gharama.
Ndani ya miezi 12, kamati ya wataalamu wa kimataifa na wawakilishi wa Vatican itatoa
mapendekezo yake katika mpango huu , chini ya uenyekiti wa Bwana Christopher Patten
a Uingereza , huku akiwa amezungukwa na Gregory Erlandson (USA), Daniela Frank (Ujerumani),
p. Eric Salobir (France), Leticia Soberon (Hispania, Mexico) na George Yeo (Singapore).
Pamoja na Msgr. Paul Tighe (Kipapa Baraza la Mawasiliano Jamii), James Ghisani (Vatican
Radio), Msgr. Carlo Maria Polvani (Katibu wa Jimbo), Msgr. Lucio Adrian Ruiz (Internet
Service Vatican) na Giovanni Maria Vian (L'Osservatore Romano).
Hatimaye,
usimamizi mpya wa timu ya IOR, wakiongozwa na Jean-Baptiste de Franssu, tangu Jumatano
9 Julai 2014, walianza utekelezaji wa hatua ya Pili ya mabadiliko , baada ya kukamilika
kwa hatua ya iliyoongozwa na mtalaam von Freyberg, kwa kutoa vipaumbelevitatu: kuimarisha
biashara ya IOR, hoja usimamizi mpya wa urithi wa mali za Vatican na rasilimali(Vam)
na shughuli zake zaidi kulenga katika kutoa huduma kwa viongozi wa dini, makanisa,
majimbo na walei wafanyakazi wa Vatican.