2014-07-09 12:09:26

Mapambano dhidi ya ukame nchini Djbouti!


Bunge la Ethiopia limepitisha makubaliano yatakayoiwezesha Ethiopia kuisaidia Djbouti kupambana na ukame unaotishia usalama wa maisha ya watu wengi. Kutokana na makubaliano haya, Djbouti itaweza kutumia mito ya maji kutoka Ethiopia kwa ajili ya shughuli za kilimo na umwagiliaji hasa kwenye Bonde la Mto Beluki, hususan kwenye maeneo ya Shinile, kilometa 100 kutoka mpakani kati ya Ethiopia na Djbouti.

Djbouti inaweza kuvuna maji ujazo wa mita 103.000 kwa siku kutoka katika mito ya Ethiopia katika kipindi cha miaka thelathini kuanzia sasa.







All the contents on this site are copyrighted ©.