Papa awaomba msamaha wote waliodhulumiwa kijinsia na watumishi wa Kanisa.
Kwenye homilia yake ya siku ya mapema Jumatatu, aliyoitoa katika Kanisa dogo la Mtakatifu
Marta ndani ya Vatican, Papa Francisko, aliyalenga maumivu ya kina ya wale wote wanaoteswa
na usaliti wa Wakatoliki, waliotenda dhambi kubwa, ya kuwanajisi watoto kingono na
madhulumu mengine ya kimwili. Katika Ibada hii kulikuwa na kundi la watu sita, kafara
wa madhulumu hayo, ambao awali walikutana na Papa Francisco , na kuzungumza naye
katika hali ya faragha, katika jengo la Wageni la ndani ya Vatican.
Papa
Francisco akiongoza Ibada hiyo , aliiangalishwa katika kuomba msamaha, na kuungana
na mateso na kilio cha kafara wote, akikumbuka mfano wa huzuni ya Petro, wakati
Yesu akipita katika mateso makali kabla ya kifo chake, macho yaliyo jaa machozi yalitazamana
na macho ya Bwana yaliyo jaa machozi ya mateso. Papa kwa ajili ya kanisa ameomba
kwa Bwana alijalie kanisa lake hisia za dhati katika huzuni na mateso ya wote waliopitishwa
katika madhulumu na unyanyasaji huu wa kutisha wa madhulumu ya ngono .
Papa
alisema, leo, moyo wa Kanisa unaonekana katika macho ya Yesu, macho ya watoto
waliofanyiwa vitendo vya kinyama na hivyo, unatazama na kuomba neema ya kuwalilia.
Kutoa kilio kwa ajili ya watoto wake, ambao ni mtima wa matumaini ya Kanisa, waliotendewa
vibaya bila hatia. Na kwa kutazama kwa kina ndani ya macho ya waathirika wa unyanyasaji,
Papa alisema, anajisikia katika moyo wake, huzuni kubwa , kwa unyanyasaji huu, alioita
kuwa ni zaidi ya kitendo kinyama kisicho elezeka.
Na kwamba inahuzunisha
zaidi , kusikia unyama huu pia unafanywa na baadhi ya watumishi wa Kanisa kama Mapadre
na Maaskofu, ambao huvunja uaminifu wao na wito wao kikuhani, na kutenda dhambi hii
kubwa. Kitendo hiki ni zaidi ya vitendo vya kujidharaulisha , ni sawa na ibada ya
kukufuru, kwa sababu watoto hawa waliokabidhiwa kwao katika karama ya kikuhani, kuwaongoza
kwa Mungu, watoto na vijana kwa udhaifu wao kimwili, wanafanywa kuwa sadaka ya
sanamu ya tamaa ya mtu. Kitendo hicho ni kunajisi sura kamili ya Mungu, sura tuliyo
umbwa nayo. Vitendo hivi vya udhalilishaji na unyanyasaji wa jinsia , hasa kwa
watoto huacha makovu ya kudumu katika maisha yao.
Katika hali ya huzuni Papa
alieleza kwa kulinganisha huzuni yake na jinsi ilivyokuwa kwa Petro, baada ya Yesu
kuhojiwa kwa vitisho, pale macho ya Petro yakiwa yamejaa machozi , yalipokutana na
macho ya Yesu anaye lia. Papa alisema , mawazo yake pia anayapeleka kwa watu wengi
wake kwa waume, wasichana na wavulana ambo macho yao yamejaa uchungu wa madhulumu
haya. Kupitia kwao, anayaona macho ya Yesu yaliyo jaa machozi, na kuomba neema hii
ya kulia kwa Bwana , neema kwa Kanisa kulia na kutoa fidia kwa wanawe na binti zake,
waliodhulumiwa vibaya, watu wasio na hatia. Papa alieleza na kuwashukuru kafara wa
dhuluma hizi walio safiri toka mbali kwa lengo la kukutana naye.
Homilia ya
Papa, iliendelea kuililia mioyo ya watoto na vijana, iliyoumizwa wakati wakitembea
katika njia ya kutaka kuelewa zaidi siri ya upendo wa Mungu na ni nia ya kukua katika
imani. Alisema, leo moyo wa Kanisa unaonekana katika macho ya Yesu kwa wavulana na
wasichana hawa. Papa alieleza kwa uchungu na ufahamu kwamba majeraha haya ni chanzo
cha maumivu ya kina ambayo hata huvunja hisia za kiroho, na hata kukata tamaa. Wengi
wa wale ambao wameteseka kwa njia hii pia hutafuta kupata msaada wa faraja katika
njia ya madawa ya kulevya. Papa alionyesha kutambua kwamba, wengi waliopita katika
uzoefu na wa madhulumu haya , pia huwa na matatizo katika mahusiano muhimu kama
wazazi, mume na mke na watoto. Mateso katika familia huwa ni makubwa, baadhi ya familia
hukabiliana hata na janga la kutisha la kifo cha mpendwa wao kujiua. Papa amezikumbuka
familia hizi, na kwa moyo wa upendo wa dhati anaungana nazo katika huzuni zao.
Na
kwa niaba ya Kanisa, ameomba msamaha wote kwa makosa na mapungufu ya viongozi wa
Kanisa walio jihami dhidi ya makosa haya na kwa matumizi mabaya ya taarifa zilizo
tolewa na wanafamilia, juu ya waathirika wa unyanyasaji. Amesema, hili lilisababisha
mateso zaidi kwa upande wa wale walioathirika vibaya na kwa hatarini watoto wengine
waliokuwa katika hatari za kukumbwa na dhuluma hii.
Kwa upande mwingine,
aliwaomba wawe na ujasiri wa kusema yote juu ya giza hili la kutisha katika maisha
ya Kanisa. Na kutangaza kwa wale wenye fikira za kufanya madhulumu haya kwamba, hakuna
nafasi hiyo , katika huduma ya Kanisa, na kani halitavumilia madhara haya kufanyika
kwa mtu yoyote awe mtoto au mtu mzima.
Papa amewataka Maaskofu wote, kufanya
huduma yao ya kichungaji kwa uangalifu mkubwa ili kusaidia kuendeleza ulinzi wa watoto,
na kuwa tayari kuwajibisha yeyote mwenye mwelekeo mpotofu, kaa Yesu alivyosema"yeyote
mwenye kumkosesha mmoja wa wadogo hawa heri afungiwe jiwe na kutupwa baharini" .