2014-07-08 14:22:15

Mapigano ya kikabila Uganda!


Serikali ya Uganda inadai kwamba, imefanya mashambulizi makubwa kwa wapiganaji wa msituni ambao wamekuwa wakiwashambulia wananchi, Magharibi mwa Uganda. Jumapili iliyopita, Kikundi cha Askari waliokuwa wamevalia kiraia kilivamia vituo vitatu ya Jeshi la Polisi na Jeshi la Uganda katika Wilaya za Ntoroko, Bundibugyo na Kasese, zinazopakana na DRC.

Idadi kamili ya watu waliofariki dunia katika tukio hili bado haijajulikana rasmi, lakini viongozi wanasema kwamba, watu kadhaa wakiwemo askari na raia wamepoteza maisha kutokana na mashambulizi haya na kwamba, zaidi ya watu tisini kadiri ya taarifa za vyombo vya habari wamefariki dunia. Mapambano haya ni kati makabila mawili yanayokalia utajiri mkubwa wa rasilimali ya nishati ya Petroli nchini Uganda.







All the contents on this site are copyrighted ©.