2014-07-06 08:34:38

Maonesho ya Sabasaba, Jijini Dar es Salaam, kumekucha!


Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amewataka wafanyabiashara nchini kuongeza juhudi za kuongeza ubora zaidi wa bidhaa zao ili ziweze kushindana na zile za nje ya nchi. Aidha Rais Kikwete amewapongeza washiriki wa maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa kwa kuongeza ubora wa bidhaa ambao kila mwaka kumekuwa na tofauti.

Kauli hiyo imetolewa na Rais Kikwete wakati akitembelea maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere jijini Dares Salaam, Jumamosi, tarehe 5 Julai 2014.

“Maonesho ya mwaka huu yamepiga hatua kubwa kwani kumekuwepo kwa ongezeko la bidhaa, bidhaa zimefungwa vizuri tukiendelea hivi tunaweza kushindana na bidhaa za kimataifa. Pendekezo langu mimi ni kuendelea kufanya ziwe vizuri zaidi,” alisema Rais Kikwete.

Akitembelea banda la Jeshi la Magereza, Rais Kikwete ambapo alijionea uzalishaji wa bidhaa za kilimo na kulitaka jeshil hilo kutoa elimu kwa wananchi juu ya kilimo bora cha kisasa. Katika ziara hiyo Rais Kikwete alitembelea mabanda mbalimbali likiwemo la Wakala wa Mafunzo nje ya nchi. Benki Kuu ya Tanzania, Bidhaa za Tanzaniana mengineyo.








All the contents on this site are copyrighted ©.