2014-07-01 10:01:18

Tusonge mbele!


Patriaki Bartolomeo wa kwanza, katika maadhimisho ya Siku kuu ya Watakatifu Petro na Paulo, Mitume iliyoadhimishwa Jumapili tarehe 29 Juni 2014, amemwandikia ujumbe wa matashi mema, Baba Mtakatifu Francisko akimwomba kutunza na kuhifadhi katika mioyo yao, matukio makuu yaliyowakutanisha hivi karibuni huko Yerusalemu na Roma, kiasi kwamba, wameimarisha urafiki na udugu pamoja na kuendeleza utashi wa kuwa na umoja kamili kadiri ya mapenzi ya Yesu Kristo mwenyewe.

Patriaki Bartolomeo wa kwanza anakumbuka hija ya kitume iliyofanywa na Baba Mtakatifu Francisko katika Nchi Takatifu, kama sehemu ya maadhimisho ya Jubilee ya miaka 50 tangu Patriaki Anathegoras na Paulo VI walipokutana na kusali pamoja, huo ukawa ni mwanzo wa mchakato wa majadiliano ya kiekumene. Anamshukuru kwa kuonesha ujasiri wa kuitisha mkutano kwa ajili ya kuombea amani huko Mashariki ya Kati. Hili ni tukio ambalo liliwakutanisha Marais kutoka Israeli na Palestina, kiasi cha kuwaacha watu wengi wakiwa wamepigwa na bumbuwazi!

Patriaki Bartolomeo wa kwanza anamwombea Baba Mtakatifu, afya ya roho na mwili, ili aweze kuendelea kutekeleza dhamana na utume wake kwa ajili ya Kanisa na ulimwengu katika ujumla wake, akiwaonjesha watu karama na upendo wake kwa Mungu na jirani!







All the contents on this site are copyrighted ©.