Mauaji ya vijana wa Israeli ni kizingiti cha amani!
Padre Federico Lombardi, Msemaji mkuu wa Vatican anaelezea kusikitishwa kwa Vatican
kutokana na mauaji ya kinyama ya vijana watu kutoka Israeli kwamba, hivi ni vitendo
ambavyo haviwezi kukubalika hata kidogo kwani ni kizingiti katika mchakato wa kutafuta
amani ya kudumu, changamoto ya kuendelea kusali na kujibidisha kutafuta amani.
Vita
inachochea vita na kusababisha chuki na uhasama. Baba Mtakatifu Francisko anaungana
na familia za wale wanaoomboleza kutokana na mauaji ya watoto wao na anamwomba Mwenyezi
Mungu mwingi wa huruma na mapendo, aweze kuwagusa watu wengi zaidi ili waoneshe moyo
wa huruma na amani.