Watiwa mbaroni kwa kujihusisha na biashara haramu ya binadamu
Watu kadhaa wametiwa mbaroni nchini Niger, Afrika ya Kaskazini kwa kujihusisha na
biashara haramu ya binadamu kutoka Nigeria. Hili ni kundi kubwa la watoto lililokuwa
linauzwa kwa watu mbali mbali nchini Niger kwa kushirikiana na wanawake kutoka Nigeria,
kadiri ya taarifa za Jeshi la Polisi la Niger.
Jeshi hili limefanya uchunguzi
wa kina na kubaini kwamba, baadhi ya wanawake kutoka Nigeria walikuwa wanajihusisha
na biashara haramu ya binadamu kutoka Nigeria. Hili ni kundi la wanawake wagumba ambao
hawakubahatika kupata watoto, kumbe wanawategemea wanawake kutoka Nigeria kuwatafutia
watoto kwa bei nafuu, lakini hatima yake, watoto hawa wanaishia kwenye mtandao wa
biashara haramu ya binadamu.
Polisi imegundua kwamba, Benin nayo iko kwenye
mkumbo wa biashara haramu ya binadamu. Jeshi la Polisi nchini Niger limewatia hatiani
wanawake 18 na kati yao kuna wanawake wa "vigogo" Serikalini.