Askofu mkuu Jozef Wesolowski avuliwa nyadhifa zake zote!
Baraza la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa limehitimisha kusikiliza kesi na hatimaye
limeamua kwamba, aliyekuwa Askofu mkuu Jozef Wesolowski, Mwakilishi wa Vatican nchini
Jamhuri ya Watu wa Domenikan kutokana na kukengeuka kwake kimaadili anavuliwa dhamana
zote kama Mkleri na hivyo tangu sasa hataruhusiwa kuendelea na utume wake kama Mkleri.
Adhabu hii itaanza kutekelezwa baada ya miezi miwili, wakati ambapo Baraza
la Kipapa la Mafundisho Tanzu ya Kanisa likiendelea kusubiri rufaa kutoka kwa Jozef
Wesolowski. Baada ya hukumu hii, utekelezaji wa kanuni zote zinazohusiana na ukubwa
wa kosa lake zitaanza kutekelezwa!