2014-06-27 08:56:44

Meriam ni mwamke kutoka Sudan aliyeitikisa dunia!


Hatimaye, baada ya kushikiliwa na kwa siku mbili na vyombo vya usalama kwenye Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Khartoum Sudan, Meriam Yeya Ibrahim Ishag, mwanamke Mkristo aliyekuwa amehukumiwa kucharazwa viboko na hatimaye adhabu ya kifo kwa kukana dini ya Kiislam ameachiliwa huru tarehe 26 Juni 2014 na sasa anahifadhiwa katika eneo lenye usalama zaidi, wakati jitihada za kumtafutia hati maalum za kusafiria zinaendelea kufanywa.

Meriam Ishag mwenye watoto wawili ameolewa na Daniel Wani, kwa sasa wana mpango wa kwenda kuishi nje ya Sudan na mipango ya kidiplomasia inaendelea ndani na nje ya Sudan.







All the contents on this site are copyrighted ©.