(Vatican Radio) Yohana Mbatizaji ni mfano kwa Wakristo leo hii. Ni wito wa Baba
Mtakatifu Francisko, Jumanne asubuhi, wakati akiongoza Ibada ya Misa aliyoadhimisha
katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta, mjini Vatican. Mahubiri yake yalilenga katika
somo la Injili, ambalo mlikuwa na maelezo juu ya Siku Kuu ya kuzaliwa kwa Yohana
Mbatizaji. Alimtaja Yohana Mbatizaji kuwa "Nabii Mkuu", akijumuisha misingi mitatu
ya wito wa Yohana Mbatizaji kwamba ni kujiandaa , kung'amua na kujishusha.
Papa
alianza kwa kueleza wito wa kwanza wa Yohana Mbatizaji kwamba, ni maandalizi. Yohana
aliiandaa njia ya Yesu bila kutaka sifa yoyote kwake mwenyewe binafsi . Watu walimtafuta
na kumfuata Yohana kwa sababu alikuwa na uwezo wa kuhubiri, na alikuwa mkweli na mtu
wazi, kwani alipoulizwa kama yeye ndiye Kristo, alijibu kwamba, kamwe siye, ila
yeye ni "sauti yake, na aliyetumwa kuandaa njia ya Bwana."
Wito wa Pili
wa Yohana Mbatizaji, Papa Francis alisema, ni kuwa ni mang'amuzi. Kutambua mambo
kwa kadiri yanavyopita. Yohana alimtambua Yesu kati ya watu waliokuwa wakipita na
kumtambulisha kuwa ndiye Masiya wa kweli .Aliwaambia wafuasi wake , kwa sauti kuu
, "Tazama huyu ndiye Mwana Kondoo wa Mungu aondoaye dhambi ya ulimwengu". Wanafunzi
walitazama , lakini Yesu aliendelea kutembea , hivyo Yohana, kwa mara ingine alirudia
kusema , “Tazama, huyu ndiye Mteule wa Mungu!" Yohana alimtambua Masiya na kumtambulisha
kwa watu wengine.
Papa aliendelea kutaja wito wa tatu wa Yohana Mbatizaji,
alijishusha, ili Bwana aweze pia kukua katika mioyo ya wengine. Alibainisha, hii
hatua ya tatu ya wito wa Yohana, ni hatua moja ngumu sana, kwa sababu tabia ya Yesu
ilikuwa tofauti na kile Yohana alichokuwa akifiri. Kabla ya kifo chake gerezani,
Yohana alijawa na mashaka na kuwatuma wafuasi wake kwa Yesu kuuliza kama kweli yeye
ndiye ni mteule. Yohana alijisikia kudhalilika kupitia kifo chake, lakini pia katika
giza la mashaka yake, bado anabaki kuwa kielelezo kwa Wakristo leo hii.
Papa
Francisko alihitimisha kwa kusema kuwa sisi Wakristo pia lazima kuandaa njia ya Bwana,
ni lazima kupata mang'amuzi juu ya ukweli na sisi lazima kuwa kujishusha ili Bwana
aweze kukua katika mioyo yetu na katika roho za watu wengine.