2014-06-25 11:41:58

Papa awasalimia wagonjwa mahujaji


Mapema Jumatano hii kabla ya Katekesi yake, Papa Francisko alikwenda katika ukumbi Paulo V1, wa mjini Vatican, kusalimia mahujaji na wageni wagonjwa, walikuwa wamekusanyika katika ukumbi huo, pia kwa lengo la kusikiliza Katekesi ya Papa.
Akisalimiana nao, Papa aliwafariji wagonjwa akisema , "muda si mrefu nitakwenda katika uwanja wa Kanisa Kuu, kukutana na umati mkubwa wa watu, mahali penye joto kali, na pia kuna hatari ya mvua kunyesha , hivyo si mahali panapofaa kwa mtu mgonjwa". Hivyo Papa aliwasihi wafuatile Katekesi yake wakiwa katika ukumbi huo kupitia screeni kubwa, iliyowekwa mbele yao. Na kwa pamoja na wagonjwa hao, walitolea sala kwa Mama Yetu Maria na kuomba baraka za Mwenyezi Mungu . Papa aliwasihi wasimsahau katika sala zao. “ Asante sana”, alimalizia.








All the contents on this site are copyrighted ©.