Majadiliano ya kidini yanapania kujenga uelewano na urafiki
Padre Miguel Angel Ayuso Guixot, Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la majadiliano ya
kidini pamoja na ujumbe wake kuanzia tarehe 22 hadi tarehe 27 Juni 2014 wako nchini
Indonesia ili kukoleza majadiliano ya kidini, kielelezo cha kuheshimiana na ujenzi
wa urafiki kati ya watu, kama anavyokazia Baba Mtakatifu Francisko. Indonesia ina
waamini wengi wa dini ya Kiislam.
Padre Guixot na ujumbe wake, wanaendelea
kukutana na kuzungumza na baadhi ya wajumbe wa Baraza la Maaskofu Katoliki Indonesia
pamoja na taasisi ambazo zinajikita katika majadiliano ya kidini. Wanatarajia pia
kukutana na kuzungumza na viongozi wakuu wa dini ya Kiislam nchini Indonesia.