2014-06-24 08:11:38

Waombeeni Wakristo huko Mashariki ya Kati!


Baba Mtakatifu Francisko katika ujumbe wake kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii, anapenda kuchukua fursa hii kuwaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kusali kwa ajili ya kuziombea Jumuiya za Kikristo huko Mashariki ya kati zinazokabiliwa na hali ngumu ya maisha, ili ziweze kuendelea kuishi mahali ambapo Ukristo umepata mizizi na chimbuko lake!

Taarifa zinaonesha kwamba, akaunti ya Baba Mtakatifu Francisko kwenye mtandao wa kijamii ujulikanao kama twitter imefikia wafuasi zaidi ya millioni kumi na nne, wanaojipambanua kwa matumizi ya lugha tisa za kimataifa. Itakumbukwa kwamba, akaunti hii kwa mara ya kwanza ilifunguliwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto XVI kunako tarehe 3 Desemba 2012.







All the contents on this site are copyrighted ©.