2014-06-24 14:53:59

Utume wa kimissionari upewe msukumo wa pekee!


Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu 23 Juni 2014 amekutana na kuzungumza na Askofu mkuu Ricardo Blazquez Peres, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Hispania pamoja na ujumbe wake kwa kuwataka waendelee kujielekeza zaidi katika kuhamasisha maisha na utume wa shughuli za kimissionari ndani ya Kanisa.

Viongozi wa Baraza la Maaskofu Katoliki Hispania, wamemwonesha Baba Mtakatifu mikakati na shughuli za kichungaji zinazotekelezwa na Kanisa Katoliki nchini Hispania. Mkazo ni kwa ajili ya kumhudumia mwanadamu: kiroho na kimwili, lakini kwa kutoa kipaumbele cha kwanza kwa maskini na wote wanaosukumiziwa pembezoni mwa Jamii.

Baba Mtakatifu amekutana na uongozi wa Baraza la Maaskofu Katoliki Hispania, uliochaguliwa hivi karibuni. Viongozi wa Baraza la Maaskofu Katoliki Hispania, wamekutana na kuzungumza pia na viongozi waandamizi kutoka Sekretarieti ya Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.