2014-06-24 10:32:33

Amani na wala si vita tena Iraq!


Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani linasema kwamba, linaunga mkono jitihada za kidiplomasia katika kutafuta muafaka na hatimaye, amani ya kudunu nchini Iraq ambayo kwa sasa inakabiliwa na machafuko makubwa ya kisiasa, kiasi cha kusababisha maafa kwa watu wasiokuwa na hatia.

Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani linasema, haliungi mkono kamwe vita huko Iraq kwani historia inaonesha kwamba, hakuna suluhu ambayo imepatikana kwa njia ya mtutu wa bunduki matokeo yake ni kwamba, watu wanaendelea kupoteza maisha siku hadi siku. Serikali ya Marekani inawajibika mbele ya wananchi wa Iraq, ili kusaidia kujenga serikali ya umoja wa kitaifa, ili wananchi wa kawaida waweze kujisikia kuwa ni sehemu ya mchakato wa maendeleo endelevu. Ili kufikia lengo hili, wananchi wote wa Iraq hawana budi kushirikishwa kikamilifu.

Uvamizi na vita iliyoendeshwa nchini Iraq kwa kusaidiana na Jeshi la Marekani limepelekea wananchi kugawanyika katika misingi ya kidini, hali ambayo imechangia kuibuka kwa watu wenye misimamo mikali ya kiimani. Tume ya haki na amani ya Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani inasema kwamba, ingependa kuona suluhu ya amani inapatika Nchini Syria, vita ambayo inaonekana kusahauliwa na Jumuiya ya Kimataifa. Majadiliano ya upatanisho wa kitaifa na misaada ya kibinadamu ni mambo msingi yanayoweza kuchangiwa na Marekani katika medani za kimataifa!







All the contents on this site are copyrighted ©.