2014-06-23 09:52:08

Homa ya Ebola, tishio kwa maisha ya watu!


Mawaziri wa afya kutoka Guinea, Sierra Leone, Liberia na Pwani ya Pembe, mwishoni mwa juma walikutana mjini Conakry, Guinea, ili kubainisha mbinu mkakati utakaotumika katika mchakato wa kudhibiti ugonjwa wa Ebola, ambao unaendelea kusababisha vifo katika maeneo yaliyoko Afrika Magharibi. Guinea ni nchi ambayo imeshambuliwa sana na ugonjwa huu tangu ulipojitokeza nchini humo, Januari 2014 na kufuatiwa na nchi za Liberia na Sierra Leone.

Watu 528 wameshambuliwa homa ya Ebola na kwamba, hadi sasa watu waliofariki dunia kutokana na ugonjwa huu ni 337. Takwimu za Shirika la Afya Duniani zinaonesha kwamba, idadi ya wagonjwa wa Ebola kutoka katika maeneo haya inazidi kuongezeka maradufu, kiasi cha kutishia usalama wa maisha kwa wananchi wanaoishi Afrika Magharibi.







All the contents on this site are copyrighted ©.