Papa Francisko kutembelea Albania nchi ya mashahidi wa imani!
Taarifa ya hija ya kitume ya Baba Mtakatifu Francisko nchini Albania hapo tarehe 21
Septemba 2014 imepokelewa kwa furaha na bashasha na waamini pamoja na watu wenye mapenzi
mema nchini Albania. Hii itakuwa ni fursa kwa Baba Mtakatifu kukutana na kuzungumza
na Jumuiya ya Waamini wa Kanisa Katoliki nchini Albania, lakini pia atapata nafasi
ya kukutana na kusalimiana na wananchi wa Albania katika ujumla wao.
Askofu
mkuu Ramiro Molinar Ingles, Balozi wa Vatican nchini Albania anasema, mwaliko kwa
Baba Mtakatifu Francisko kutembelea nchini Albania ulitolewa na viongozi wa Kanisa
na Serikali nchini Albania, wakati Waziri mkuu wa Albania Bwana Edi Rama alipotembelea
Vatican mwezi Aprili, 2014. Hii itakuwa ni hija ya kwanza ya kitume kufanywa na Baba
Mtakatifu Francisko katika nchi za Ulaya.
Baba Mtakatifu anatembelea Albania
kama nchi ambamo Wakristo wengi wanajisadaka kwa ajili ya Kristo na Kanisa lake na
damu yao imekuwa ni chemchemi ya kukua na kuenea kwa Injili. Atatembelea Albania mahali
ambako majadiliano ya kidini na kiekumene yanaendelea katika uhalisia wa maisha ya
watu. Baba Mtakatifu atatembelea Albania kwa siku moja, lakini hata hii inatosha kuwaimarisha
ndugu zake katika imani na mapendo kwa Kristo na Kanisa lake