2014-06-13 07:48:11

Majembe mapya Vikarieti ya Tanzania!


Wamissionari wa Shirika la Damu Azizi ya Yesu, Vikarieti ya Tanzania wamehitimisha mkutano mkuu wa uchaguzi uliokuwa unafanyika Jimboni Dodoma na kusimamiwa na Padre Oliviero Magnone, mkuu wa Shirika la Wamissionari wa Damu Azizi ya Yesu Kanda ya Italia. Majembe yaliyochaguliwa kuliongoza Shirika katika kipindi hiki cha mpito kwa Tanzania kuwa Jimbo kamili linalojitegemea ifikapo mwaka 2015.

Waliochaguliwa kwenye mkutano mkuu wa tano wa Shirika la Wamissionari wa Damu Azizi ya Yesu Vikarieti ya Tanzania ni:

Padre Reginald Mrosso, C.PP.S. Mkuu wa Shirika.
Padre Gregory Mkhotya, C.PP.S. Makamu mkuu wa Shirika.
Padre Egidius Seneda, C.PP. S. Katibu mkuu.
Padre Francis Bartoloni, C.PP.S. Mshauri.
Padre Richard Kungi, C.PP.S. Mtunza fedha.







All the contents on this site are copyrighted ©.