2014-06-12 12:41:29

Papa apendekeza mashindano ya kombe la Dunia iwe ni Siku Kuu ya amani duniani


Baba Mtakatifu Francisko, amepeleka ujumbe wa matashi mema kwa njia ya video kwa washiriki wote wa michezo ya mashindano ya kombe la Dunia la Mpira wa miguu, yanayotazamiwa kuanza hivi karibuni, Brazil.
Amesema, "napenda kutuma salamu zangu za dhati kwa waandaaji, wafanikishaji na kwa kila mwanamichezo na mashabiki, pia kwa watazamaji wote wa njia ya televisheni, radio na internet, na washiriki wote wa tukio hili linalovuka mipaka yote ya lugha, utamaduni na kitaifa. Katika ukweli, mpira wa miguu una tunu nyingi katika mahusiano ya binadamu hivyo si mashindano tu lakini pia huwa na manufaa katika mitazamo mingine ya kimaisha , na hasa katika ujenzi wa haki na amani. Michezo ni shule ya amani , hufundisha uvumilivu katika kujenga amani".

Papa ameonyesha matumaini yake kwamba, pamoja na maadhimisho ya michezo ya Kombe la mpira wa miguu la Dunia, pia madhumuni yake yanaweza kubadilishwa na kuwekwa kama ni Siku Kuu ya Mshikamano kati ya watu.
Katika ujumbe huu, Papa anasema Michezo si tu wakati wa kujifurahisha , lakini pia ni huonyesha jinsi binadamu anavyoweza kushirikiana katika kukuza tunu msingi za katika utu wa mtu, na ujenzi wa amani na maelewano na umoja . Na hivyo mashindano ya mpira wa miguu licha ya kuwa tu aina ya burudani, lakini pia alisisitiza Papa, inakuwa ni nyenzo ya kuonyesha uadilifu ambamo utu na uzuri wa binadamu hukuzwa na kusaidia kujenga amani zaidi na mshikamano na udugu. Katika michezo, tunaona kwamba inawezekana kuishi kwa uaminifu, uvumilivu, urafiki, kugawana, kushirikishana na mshikamano. Kwa kweli, mpira wa miguu hufufua uadilifu kwa wengi na si tu wakati wa mashindano ya mpira kwenye uwanja wa mpira , lakini pia katika nyanja zote za maisha, hasa zaidi katika ujenzi wa amani.
Papa anaendelea kusema, michezo ni shule ya amani, inatufundisha kujenga amani, kupitia kujifunza kutunza uaminifu haki na kuheshimiana, kati ya wapinzani. Michezo hutufundisha kwamba , ni lazima kufanya bidii katika kupata mafanikio ya kuwa mshindi . Kwa namna hiyo, tunaweza kuona mchezo huu wa mpira wa miguu, kama mfano katika utendaji wa maisha yetu. Katika maisha ni muhimu kupambana, kujitahidi kupata matokeo mazuri. Kiroho, michezo hutukumbusha, mfano wa kuongeza bidii katika majitoleo kama sadaka muhimu ya kukua katika fadhila na majiundo ya tabia ya mtu. Ni lazima kuwa na mafunzo makali kwa ajili ya kumboresha mtu katika uchezaji wake na hivyo ndivyo anavyokua katika ahadi zake za kuwa mwaminifu , adilifu na mtu wa haki na amani kati kati ya watu na watu wema!

Mpira wa miguu, unaweza na inapaswa kuwa shule kwa ajili ya majiundo ya kujenga utamaduni wa kukutana, wenye kuleta maelewano na amani miongoni mwa watu.
Na hapa tunapata somo la pili juu ya mchezo, kwmba ni kucheza kwa haki. Kucheza kama timu kunahitaji ufahamu zaidi ya yote ni kwamba , kwanza ni kwa ajili ya manufaa ya timu zima, na si kwa manufaa binafsi. Katika kupata ushindi ni lazima kuushinda ubinafsi, ubinafsi katika kila hali na kila aina ya ubaguzi, iwe kikabila, kimbali , rangi, utaifa n.k . Badala yake ni uvumilivu na kutunza utu wa mtu, kwa kuwa ubinafsi katika mpira wa miguu ni kikwazo kwa mafanikio ya timu; na ndivyo ilivyo , kama tunakuwa na ubinafsi katika maisha, kwa kuwapuuza watu walio karibu nasi, tunaumiza jamii nzima.

Papa aliendelea kutaja somo la mwisho la michezo ya kufikia amani, ni heshima sahihi kati ya wapinzani. Alieleza siri ya ushindi, iwe uwanjani au katika maisha, iko katika kujua jinsi ya kumheshimu mchezaji mwingine, hata kama ni mpinzani wetu. Hakuna mafanikio katika ubinafsi, iwe uwanjani, au katika maisha! Na kwamba, wanaojitenga hujisikia kutengwa! Na, kama ulivyo ukweli kwamba, mwishoni mwa mashindano, timu moja hupata ushindi , kama ilivyo katika mashindano haya ya Kombe la Mpira wa miguu la Dunia, ni timu ya taifa moja tu itakayoinua kikombe juu kama mshindi. Lakini katika ukweli, washiriki wote wa mashindano haya ni washindi katika kuwa adilifu, na katika kudumisha haki na umoja. wote ni washindi katika uimarishaji wa uimarishaji wa viungo vya umoja na mshikamano wa binadamu.

Papa alimalizia hotuba yake, kwa kumshukuru Rais wa Brazil, Bi Dilma Rousseff, kwa salaam zake, na alimhakikishia kwamba anatolea sala zake kwa Mungu ili mashindano haya ya Kombe la Dunia yafanyike kwa kila utulivu, kuheshimiana, mshikamano na udugu kati ya wake kwa waume, wakijitambua kama ni watu wa familia moja. Asante.








All the contents on this site are copyrighted ©.