Bara la Afrika linaendelea kucharuka kiuchumi! Lakini Pochi hakuna!
Licha ya majanga mbali mbali yanayoendelea kujitokeza nchini Nigeria, lakini bado
Nigeria inaendelea kucharuka katika masuala ya kiuchumi na kwamba, inaonekana kuwa
na mvuto mkubwa kwa wawekezaji kutoka Barani Ulaya na Marekani. Utafiti uliofanywa
na Jarida la kiuchumi lijulikanalo kama Wall Street Journal, kuhusu mwenendo wa soko
katika masuala ya uchumi. Kati ya nchi 20 zinazoendelea kuibukia katika masuala ya
kiuchumi, kuna nchi 11 kutoka Barani Afrika.
Takwimu hizi zinaonesha kwamba
nchi zinazoongoza kutoka Afrika ni kama ifuatavyo: 1. Nigeria ni nchi ya kwanza
kwa kuwa na asilimia 29.5%. 2. Kenya inayochukua nafasi ya tano kwa kuwa na asilimia
23.17%. 3. Angola inachukua nafasi ya sita kwa kuwa na asilimia 21.9%. 4. Ghana
inachukua nafasi ya tisa kwa kuwa na asilimia 18. 73%. 5. Ethiopia inachukua nafasi
ya 11 ikiwa na asilimia 17. 27%. 7. Morocco inashikilia nafasi ya 12 ikiwa na asilimia
16.79. 8. Tanzania inashikilia nafasi ya 13 kwa kuwa na asilimia 16.79. 9. Algeria
inashikilia nafasi ya 14 kwa kuwa na asilimia 16.06%. 10. Pwani ya Pembe inashikilia
nafasi ya 16 kwa kuwa na asilimia 14.58. 11. Zambia inashikilia nafasi ya 17 kwa
kuwa na asilimia 13.63%. 12. Uganda inashikilia nafasi ya 19 kwa kuwa na asilimia
13.14.
Taarifa hii inaonesha mwelekeo wa uwekezaji kutoka katika makampuni
ya kimataifa yanayotaka kuwekeza Barani Afrika. Kiashilia kinaonesha ni asilimia kiasi
gani wawekezaji kutoka nje wamevutiwa na nchini husika. Ikiwa kama idadi ya Makampuni
ya Kimataifa 50 kati ya 200 yanaonesha kuvutiwa na nchi husika, nafasi yake ni 25%.
Makampuni makubwa ya kimataifa yanaendelea kuonesha nia ya kuwekeza Barani Afrika
ili kushiriki katika mchakato wa maendeleo ya watu wa Bara la Afrika.
Mradi
wa umeme Barani Afrika uliotangazwa na Serikali ya Marekani utanufaisha watu millioni
240 kutoka Barani Afrika katika nchi za: Ethiopia, Ghana, Kenya, Nigeria, Liberia
na Tanzania. Mwezi Agosti kunatarajiwa kufanyika kwa Jukwaa la Maendeleo kati ya Bara
la Afrika ya Singapore, ili kuimarisha ushirikiano katika masuala ya biashara kati
ya Afrika ya Nchi kutoka Asia.