Shukurani zatolewa kwa Papa Francisko kwa kuitisha Mkutano wa sala
Rais Shimon Peres wa Israel , na pia Rais Mahmoud Abbas wa Palestina, Jumapili wakishiriki
katika Mkutano wa sala ulioitishwa na Papa Francisko, wote wawili walionyesha moyo
wa shukurani kwa Papa Francisko, kwa mwaliko wake wa kuwataka wafike Vatican katika
tarehe hii 8 June 2014. Lengo kuu la mkutano huu ikiwa ni kujiweka chini ya Miguu
ya Bwana, Mungu mmoja, na kuomba amani kati ya Israel na Palestina na Mashariki
ya kati yote. Hotuba za Marais wawili pia zilitoa shukurani kwa hotuba nzuri iliyotolewa
na Papa Francisko.
Rais wa Israel, katika hotuba yake amemtaja Papa kuwa
mjenzi wa madaraja ya udugu wa aman. Na pia ilirejea maombi ya Papa ,ambamo alisisitiza
haja kwa kila mmoja kufanya kazi kwa ajili ya kufikia amani, hata kwa gharama ya
sadaka na maafikiano, na bila kukata tamaa hata kama inaonekana kuwa ni njia ndefu
kuifikia amani kamili. Lakini ni kusonga mbele na njia hiyo kwa manufaa ya sasa na
kwa vizazi vipya.
Rais Peres alionyesha imani yake kwamba, ukweli, watu wote
wa Israel na pia Palestina, wana hamu kubwa ya kumkumbatiana kwa amani. Na alitaja
Machozi ya akina mama juu ya watoto wao waliopoteza maisha, kumbukumbu hiyo bado,
inararua mioyo ya watu wenye mapenzi mema. Hivyo, iwqapo kila mmoja ana hamu hiyo,
basi inakuwa ni jambo la azima kukomesha kelele za vurugu, migogoro. Rais Peres
alisisitiza, watu wote wanahitaji amani. Amani yenye kuheshimiana, usawa na uhuru.
Na Rais wa Mamlaka ya Palestina, Mahmound Abbbas, hotuba yake ilisisitiza
zaidi uwepo wa utambuzi wa kweli wa amani ya haki kwa watu wa Palestina, iwe Waislamu,
Wakristo na Wayahudi . Alisema wote wanataka amani na maisha ya kuheshimiana na
uhuru, uhuru wenye kuwawejesha kustawi katika nchi yao na kujitegemea. Rais Abbas
alieleza na kunukuu maelezo ya Mtakatifu Yohana Paulo II, aliposema, "iwapo amani
itafanikishwa Yerusalemu , amani itashuhudiwa katika dunia nzima".
Kwa hiyo
, Rais Abbas kwa lugha ya Kiarabu akasema, , na tumwombe Bwana, amani katika Nchi
Takatifu, Palestina na Yerusalemu, pamoja na watu wake. Tunakuomba Bwana, uijalie
Palestina na Yerusalemu hasa, iwe eneo la salama kwa waumini wote, na mahali pa sala
na ibada kwa wafuasi wa dini tatu zinazosadiki kwa Mungu mmoja.
Katika mkutnao
huu wa maombi kwa ajili ya amani Mkoa wa Mashariki ya Kati,viongozi hawa watatu Papa,
Marais wa Palestina na Israel, waliufunga kwa ishara ya amani kwa kumkumbatiana
kirafiki na kwa kupanda mti wa mzeituni wa amani ndani ya Bustani za Vaican, kama
kumbukumbu kwa tukio hili la kihistoria.