2014-06-05 08:37:09

Dakika moja ya kuombea amani Mashariki ya Kati!


Mahali popote pale utakapokuwa wakati wa kusherehekea Siku kuu ya Pentekoste, itakapo gota saa 7: 00 mchana, inamisha kichwa chako, sali kidogo kwa ajili ya kuombea amani Mashariki ya Kati, kadiri ya imani na Mapokeo yako ya kidini ukiwa umeungana na Baba Mtakatifu Francisko. Ni changamoto inayotolewa na Baraza la Maaskofu Katoliki Argentina.

Waamini na watu wote wenye mapenzi mema wanaalikwa kwa namna ya pekee, kusali kwa ajili ya kuombea jitihada za Baba Mtakatifu Francisko kwa ajili ya upatikanaji wa amani huko Mashariki ya Kati. Itakumbukwa kwamba, Baba Mtakatifu Francisko atakutana na kusali pamoja na Marais kutoka Palestina na Israeli kama sehemu ya utekelezaji wa mwaliko kwa viongozi hawa wawili wakati wa hija yake ya kitume katika Nchi Takatifu.

Baraza la Maaskofu Katoliki Italia linawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema, wakati wa Maadhimisho ya Sherehe ya Pentekoste kusali kwa ajili ya kuombea amani huko Mashariki ya Kati.







All the contents on this site are copyrighted ©.