2014-06-04 10:10:50

Radio za Kimataifa kurusha matangazo ya dharura!


Radio Vatican ambayo ni mwanachama wa Shirikisho la Kimataifa linaloratibu matangazo ya Radio kwa masafa mafupi lijulikanalo kama (HFCOC: High Frequnecy Co-ordination Conference), imeridhia kushiriki katika mchakato wa kutengeneza Radio itakayokuwa na uwezo wa kurusha matangazo yake kwa njia ya masafa mafupi wakati wa dharura na maafa asilia.

Katika mkutano wa Shirikisho hili unaofanyika mjini Jakarta, Indonesia kati ya tarehe 5 - 6 Juni 2014, Radio zote za kimataifa zinazorusha matangazo yake kwa kutumia masafa mafupi zitaridhia mwaliko huu, ili kuhamasisha Jumuiya ya Kimataifa na Jamii kwa ujumla umuhimu wa kuwa na kituo cha radio Kimataifa kitakachorusha matangazo yake katika masafa mafupi, kikiwa tayari na vifaa vinavyoweza kutumika katika dharura, ili kuwasaidia watu ambao wanaweza kujikuta katika maafa.

Radio Vatican inatarajia kurusha matangazo ya dakika 30:00 ambayo yameandaliwa na BBC kwa ajili ya lengo hili katika maeneo ya Bara la Asia katika masafa ya 2184o khz katika masaa 05:00 na saa 5:30 UTC.







All the contents on this site are copyrighted ©.