2014-06-03 08:10:11

Vinara wa ndoa za utotoni Afrika!


Shirika la kuhudumia la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Watoto wadogo UNICEF kwa kuungana na UNFPA yana unga mkono kampeni iliyozinduliwa hivi karibuni ya Umoja wa Nchi za Kiafrika ya kupambana na ndoa za utotoni ambazo zinazidi kuongezeka kwa wingi Barani Afrika na hivyo kusabababisha majanga makubwa kwa watoto zaidi ya millioni 17 wanaotoka Barani Afrika.

Takwimu zinaonesha kwamba, Niger, Chad, Jamhuri ya watu wa Afrika ya Kati, Guinea, Msumbiji, Mali, Burkina Faso, Sudan ya Kusini na Malawi zinaongoza kwa ndoa za utotoni Barani Afrika. Changamoto hii iliyotolewa na Umoja wa Afrika inapaswa kuungwa mkono na wapenda amani duniani anasema Bwana Martin Mogwanja, Mkurugenzi msaidizi wa UNICEF wakati akichangia mada kwenye mkutano uliofanyika hivi karibuni mjini Addis Ababa.

Kampeni hii iwasaidie watoto kukua na kukomaa hadi watakapofikia umri wa miaka kumi na minane inayoruhusiwa kisheria kuweza kufanya maamuzi kuhusu maisha yao badala ya kudumazwa katika ndoa za utotoni ambazo zimeendelea kuwa na madhara makubwa kwa watoto hawa na familia wanazounda! Kwa mara ya kwanza katika historia, Jumuiya ya Kimataifa inaonesha utashi wa kutaka kupambana na ndoa za utotoni ili kuimarisha afya, matumaini na haki msingi za watoto Barani Afrika.

Kampeni hii iliyozinduliwa hivi karibuni itadumu kwa kipindi cha miaka miwili katika ngazi ya kitaifa kwa mataifa kumi. Lengo ni kuwawezesha wananchi kufahamu madhara ya ndoa za utotoni na hivyo wanasiasa na vyombo vya sheria kuwajibika ili kukomesha vitendo hivi.








All the contents on this site are copyrighted ©.